Mwenyekiti Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete akimkabidhi moja ya vitendea kazi, Mwenyekiti mpya wa CCM, Rais Dk. John Magufuli baada ua Wajumbe wa mkutano Mkuu wa CCM, kumpitisha asilimia kwa mia ya kura, katika kumchagua jana katika ukumbi wa Dodoma Convention.
Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Rais mstaafu Jakaya Kikwete akimpongeza Mwenyekiti mpya wa CCM Rais Dk. John Magufuli baada ya wajumbe wa Mkutano Mkuu maalum wa CCM kumchagua kwa kura asilimia mia kwa mia.
Mweneyekiti wa CCM mstaafu Rais Mstaafu Jakaya Kikwete na Mwenyekiti Mpya wa CCM Rais Dk. John Magufuli wakipunga mkono baada ya Magufuli kutawazwa rasmi kushika nafasi hiyo jana mjini Dodoma.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein akimpongeza Rais Dk John Magufuli baada ya kutawazwa rasmi kuwa Mwenyekiti mpya wa CCM lo mjini Dodoma. Katikati ni Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Rais Mstaafu Jakaya Kikwete
Mwenyekiti mpya wa CCM, Rais Dk. John Magufuli akitoa hotuba yake, baada ya kutawazwa kushika nafasi hiyo kwa kupata kuta asilimia mia kwa mia zilizopigwa na wajumbe wa mkutano mkuu maalum wa CCM uliofanyika jana mjini Dodoma. (Picha zote na Bashir Nkoromo)





No comments:
Post a Comment