Pages

Tuesday, April 5, 2016

Serikali yahaidi kuboresha usikivu wa Shirika la utangazaji la taifa Mikoa ya pembezoni

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Zelote Stephen (kulia) pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Mhe. Mathew Sedoyeka (kushoto) wakiteta jambo na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye baada ya kuwasili katika Mkoa wa Rukwa jana kuzungumza na wadau wa sekta anazosimamia. (Picha zote na Genofeva Matemu- Maelezo, Rukwa)
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akizungumza na viongozi wa CCM Mkoa wa Rukwa jana wakati wa ziara yake mkoani humo kukutana na wadau wa sekta anazozisimamia. Kushoto kwa Waziri ni Mwenyekiti wa CCM Rukwa Bw. Hypolitus Matete. 
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Zelote Stephen (kushoto) akuzungumza na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye alipofika ofisini kwake wakati wa ziara ya kukutana na wadau wa sekta ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na kutoa vitendea kazi kwa maafisa mawasiliano jana Mkoani Rukwa. 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akizugumza na watendaji kutoka Mkoa wa Rukwa pamoja na wadau wa kada za Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo alipokutana nao jana Mkoani hapo kujadili mambo mbalimbali katika sekta hizo pamoja na kutoa vitendea kazi kwa maafisa mawasiliano. 
Baadhi ya watendaji kutoka Mkoa wa Rukwa pamoja na wadau wa kada za Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wakimsikiliza kwa makini Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (hayupo pichani) alipofanya ziara yake jana Mkoani Rukwa  kujadili mambo mbalimbali pamoja na kukagua ofisi za TBC na kutoa vitendea kazi kwa Maafisa Mawasiliano wa Mkoa wa Rukwa. 
Mwamuzi na Mkufunzi wa mchezo wa netibali Mkoa wa Rukwa Bibi. Louisa Monji akichangia wakati wa kikao na  Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye alipofanya ziara katika mkoa huo jana kujadili mambo mbalimbali pamoja na kukagua ofisi za TBC na kutoa vitendea kazi kwa Maafisa Mawasiliano wa Mkoa wa Rukwa. 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akiikagua iPad kabla ya kumkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Zelote Stephen (kushoto) kwa ajili ya kuboresha utendaji kazi kwa maafisa mawasiliano waliopo Mkoani hapo. Mhe. Nnauye alikabidhi iPad tatu kwa Mkoa wa Rukwa jana baada ya kufanya ziara fupi na kuonana na wadau wa sekta anazozisimamia. 
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mhe. Iddi Kimanta akitoa taarifa fupi kuhusu sekta za Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo  kwa Waziri wa sekta hizo Mhe. Nape Moses Nnauye alipofanya ziara Wilayani hapo jana Mkoani Rukwa. 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akizungumza moja kwa moja kupitia radio ya Wilaya Nkasi FM alipofanya ziara katika radio hiyo kuona mafanikio yaliyoletwa na Wilaya ya Nkasi kwa kuwa na radio ya Wilaya.

Na Genofeva Matemu – Maelezo, Rukwa
05/04/2016
SERIKALI imeamua kuwekeza kwenye mikoa ya pembezoni kuhakikisha usikivu wa shirika la utangazaji la taifa unakua mkubwa na wakutosha kwa kuweza kusikika katika maeneo yote nchini. 

Rai hiyo imetolewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye alipofanya ziara jana katika Mkoa wa Rukwa na kukagua mitambo ya kurushia matangazo ya shirika la utangazaji la taifa pamoja na kukutana na wadau wa sekta anazozisimamia.

“Mkoa wa Rukwa ni kati ya Mikoa ya pembezoni ambayo usikivu wa shirika la utangazaji la taifa ni mdogo hivyo kufanya mikoa hii kusikiliza matangazo ya redio kutoka nchi jirani badala ya kusikiliza taarifa za nchi yetu” alisema Mhe.  Nnauye. 

Akizungumza wakati wa ziara hiyo Mhe. Nnauye amesema kuwa lengo la serikali ni kuwa na vyombo vyenye nguvu ya kusikika mikoa ya pembezoni na ikiwezekana viweze kuvuka mipaka na kusikika katika mikoa ya jirani  badala ya sisi kusikiliza matangazo kutoka katika vyombo vyao.

Ili kutimiza lengo hilo Mhe. Nnauye amehaidi kufanya maamuzi magumu kwa kusimamia ubadilishaji wa baadhi ya vifaa, kuhamishia mitambo maeneo ya milimani pamoja na kuweka busta zenye nguvu zitakazoweza kufikisha matangazo ya redio na televisheni ya taifa nchi nzima.

Akitoa taarifa kuhusu usikivu wa shirika la utangazaji la taifa Mkoa wa Rukwa Kaimu Mkuu wa Kanda TBC nyanda za juu kusini Bw. Hosea Cheyo amesema kuwa usikivu wa shirika la utangazaji la taifa upo kwa asilimia sabini na tano tu hivyo kuiomba serikali kuhamisha mtambo wa shirika hilo katika mlima wa king’ombe ili wananchi wa Mkoa wa Rukwa waweze kupata fursa ya kusikiliza radio ya taifa. 

Naye Meneja wa TCRA Kanda ya nyanda za juu kusini Eng. Lilian Mwangoka ameipongeza Halmashauri ya Nkasi iliyopo katika Mkoa wa Rukwa kuwa na redio ya wilaya ijulikanayo kama Nkasi FM inayosaidia kufikija taarifa kwa jamii na kuzitaka Halmashauri zingine nchini kuiga mfano wa Nkasi kwa kufungua redio za Halmashauri zitakazowasaidia kujua yale yote yanayoendelea duniani.

No comments:

Post a Comment