TANGAZO


Saturday, April 30, 2016

MKUSANYIKO WA KUMUENZI MAREHEMU ANDREW NICKY SANGA KUFANYIKA LEO TAREHE 30.04.2016 TRIPLE 7 KAWE

Ndugu zetu pamoja na Marafiki zetu, wakati huu tukiendelea kuomboleza msiba wa mpendwa wetu Andrew Nicky Sanga, tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa ushiriki wenu wa hali na mali katika kuandaa safari yake ya mwisho.

Katika kumuenzi na kukumbuka urafiki wake wa kipekee, Kamati ya Maandalizi ya Dar es Salaam inawaalika na kuwakaribisha katika kusanyiko la kumuenzi jioni ya tarehe 30 April 2016 kuanzia saa 11 jioni pale Triple 7 (@777).


Kusanyiko hili ni mahsusi kwa mambo mawili makubwa, moja likiwa ni kukumbuka na kuenzi maisha yake katikati yetu na pili kupashana habari za kuhitimisha maandalizi ya Safari ya kumuweka katika nyumba yake ya Milele.

Naomba tujumuike wote na tunaamini hata huko aliko atafurahi tunapomkumbuka.

Bwana ametoa na Bwana Ametwaa Jina la Bwana Lihimidiwe 
Imetolewa na Dr. George Longopa
KNY Kamati ya Maandalizi ya Dar ES SALAAM
Simu 0754 870969

No comments:

Post a Comment