TANGAZO


Thursday, March 10, 2016

Serikali ya Kifalme ya Norway kusaidia ukusanyaji wa kodi nchini Tanzania



Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Kifalme ya Norway, Tone Skogen akizungumza wakati wa ufuzinduzi wa mpango wa kuboresha ukusanyaji kodi nchini Dar es Salaam leo. Serikali ya nchi hiyo imetoa Dolla za Kimarekani milioni 5 kwa ajili ya uboreshaji huo. Kushoto ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Ashatu Kijaji. (Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Ashatu Kijaji, akizungumza wakati wa mkutano wa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Norway kwenye uzinduzi wa mpango wa kuboresha ukusanyaji kodi nchini, Dar es Salaam leo. Kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Kifalme ya Norway, Tone Skogen. 
Baadhi ya waandishi wa habari, wakiwa katika  uzinduzi wa mpango huo, wa kuboresha ukusanyaji kodi nchini, kati ya Serikali ya Tanzania na Norway, jijini Dar es Salaam leo. 
Baadhi ya Maofisa wa TRA na wa Wizara ya Fedha wakiwa katika mkutano huo, wa pamoja katika ya Serikali ya Tanzania na Norway katika uzinduzi wa mpango wa kuboresha ukusanyaji kodi nchini,  jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya waandishi wa habari, wakiwa katika  uzinduzi wa mpango huo, wa kuboresha ukusanyaji kodi nchini, kati ya Serikali ya Tanzania na Norway, jijini Dar es Salaam leo.
Waandishi wa habari, wakichukua habari, wakati wa uzinduzi wa mpango huo, wa ushirikiano wa kuboresha ukusanyaji kodi nchini, kati ya Serikali ya Tanzania na Norway, jijini Dar es Salaam leo.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Ashatu Kijaji, akifafanua jambo wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari katika mkutano huo, wa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Norway kwenye uzinduzi wa mpango wa kuboresha ukusanyaji kodi nchini, jijini Dar es Salaam leo. Serikali ya Norway imetoa Dolla za Kimarekani milioni 5 kwa ajili ya uboreshaji huo. Kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway, Tone Skogen.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Ashatu Kijaji, akifafanua jambo wakati wa mkutano wa uzinduzi wa mpango wa kuboresha ukusanyaji kodi nchini, jijini Dar es Salaam leo. 
Kaimu Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alphayo Kidata, akitoa ufafanuzi kwa wandishi wa habari, wakati wa mkutano huo. Katikati ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji na kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Kifalme ya Norway, Tone Skogen.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Ashatu Kijaji, akifafanua jambo wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari wakati wa  mkutano huo.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Ashatu Kijaji (kushoto), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Kifalme ya Norway, Tone Skogen (kulia), Kaimu Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alphayo Kidata (wa pili kushoto) na Balozi wa Norway nchini, Hanne-Marie Kaarstad (wa pili kulia), wakizungumza jambo wakati wa mkutano huo. 
 
Na Beatrice Lyimo-MAELEZO

10/03/2016

Dar es Salaam

SERIKALI ya Kifalme ya Norway imetoa kiasi cha Dolla za kimarekani milioni 5 kwa Serikali ya Tanzania kwa kuwaunga mkono Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Serikali ya awamu ya tano katika jitihada zake katika kuimarisha ukusanyaji wa mapato nchini.


Makubaliano hayo ya ufunguzi wa kuchangia mapato yamefanyika leo jijini Dar es salaam kati ya Naibu Waziri wa mambo ya Nje kutoka Serikali ya Kifalme ya Norway Mhe. Tone Skogen pamoja na Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt Ashatu Kijaji.


Akizungumza katika ufunguzi huo Naibu Waziri wa Mambo ya Nje kutoka Serikali ya Kifalme ya Norway Mhe. Tone Skogen amesema kuwa lengo la mpango huo ni kuimarisha na kuongeza kodi ya mapato ya ndani kwa  kuhakikisha kwamba mianya ya wakwepaji kodi inazuiwa.


Kwa upande wake Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt Ashatu Kijaji amesema kuwa Serikali imeendelea kuimarisha na kuwaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa ulipaji kodi bila kushurutishwa ili kuondokana bajeti  tegemezi kutoka nje.


“Lengo la kuimarisha uelewa wa wananchi kuhusu umuhimu wa  ulipaji kodi bila kushurutishwa na kuzuia mianya yote ya ukwepaji kulipa kodi  ni kuondokana na utegemezi wa bajeti na kuanza kujitegemea hivyo hatuwezi kufika huko bila kuimarisha ukusanyaji wa  mapato nchini” alisisitiza Naibu Waziri huyo.


Naye Kaimu Kamishna Mkuu TRA Bw. Alphayo Kidata ameishukuru Serikali ya Kifalme ya Norway kwa kuimarisha uwezo wa wataalamu nchini kwa kuwawezesha  mbinu mbalimbali za kukagua mahesabu katika makampuni makubwa nchini.


Awali Serikali ya Kifalme ya Norway ilitoa zaidi ya Dola za kimarekani million 3 katika mpango huo wa kuimarisha ukusanyaji wa mapato nchini.

No comments:

Post a Comment