Jopo la waamuzi mjini Florida limempatia aliyekuwa nyota wa mchezo wa mieleka Hulk Hogan kitita cha dola milioni 115 kama malipo baada ya mtandao mmoja wa udaku Gawker kuchapisha kanda moja ya ngono ya mchezaji huyo ambaye amestaafu.
Kanda hiyo ya video ilichapishwa mwaka 2012 baada ya Hogan kurekodiwa akifanya ngono na mke wa rafikiye.
Mawakili wa Gawker walihoji kwamba ijapokuwa jopo la waamuzi huenda ukavichukia vitendo vya mtandao huo,swala la uhuru wa vyombo vya habari ni muhimu sana.

No comments:
Post a Comment