Mwenyekiti wa Jukwaa
la wahariri Bw.Absalom Kibanda akiwahimiza wahariri wa vyombo vya Habari (hawapo pichani)
kuhusu kutenda wajibu wao wakati wote wanapofanya kazi zao kwani uhuru waendana na wajibu leo jijini
Dar es Salaam. Kulia kwake ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa
na Michezo Mhe. Nape Nnauye na wamwisho ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu Idara ya Habari-Maelezo, Zamaradi Kawawa.
Mhariri Mkuu wa Gazeti
la The Guardian Bw. Jesse Kwayu akichangia hoja wakati wa kikao kati ya wahariri wa vyombo vya habari na
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe Nape Nnauye. Bw. Kwayu alimsihi Mhe. Nape
kuzidi kuwa karibu na waandishi na pia zitungwe sheria zitakazo wawezesha waandishi wa habari kupata habari kwa urahisi na kufanyakazi yao ya kuhabarisha jamii.
Mhariri
Mtendaji wa magazeti ya Jamhuri Media Ltd Bw. Deodatus Balile akichangia hoja katika kikao kati ya wahariri wa vyombo vya habari na
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa naMichezo.
Mhariri
wa Gazeti la the Citizen Bw. Peter Nyanje akichangia jambo wakati wa kikao kati ya wahariri wa vyombo vya habari na
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akiongea na wahariri wa Vyombo vya Habari
(hawapo pichani) leo hii jijini Dar es Salaam. Mhe Nape alivipongeza vyombo vya
Habari kwa kufanya wajibu wao katika kipindi cha uchaguzi mkuu na kuwahaidi kuwa
Serikali itakuwa karibu nao sana na kuhimiza kuwa serikali ya awamu ya Tano itatunga sheria nzuri itakayo rahisisha utekelezaji wa majukumu yao.Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Jukwaa
la wahariri Bw. Absalom Kibanda. Picha na Daudi Manongi-), Wizara ya habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo(WHUSM).


No comments:
Post a Comment