TANGAZO


Monday, December 7, 2015

Obama: Shambulio la California lilikuwa la kigaidi

Obama


Image copyrightReuters
Image captionObama amesema vita dhidi ya ugaidi havifai kuwa vita kati ya Wamarekani na Waislamu

Rais Barack Obama amelihutubia taifa la Marekani kufuatia shambulio la risasi la wiki iliyopita katika jimbo la California ambalo lilisababisha vifo vya watu 14.
Rais Obama amesema wazi kwamba hakuna ushahidi kwamba muuaji alikuwa anatekeleza mauaji hayo kwa maelekezo ya kundi lolote kutoka nje ya Marekani .
Huku akisisitiza kusema kwamba lilikuwa ni shambulio la kigaidi hivyo ni muhimu kupambana nalo, na suala hili lisionekane kama ni vita baina ya Marekani na waislamu bali ni kwa waislamu weye itikadi kali za kigaidi.

No comments:

Post a Comment