Watu nchini Uturuki wanapiga kura hii leo katika duru ya pili ya uchaguzi wa ubunge ndani ya miezi mitano.
Chama cha AK cha rais Recep Tayyip Erdogan kilishindwa kupata wingi wa viti kwenye uchaguzi wa mwezi Juni na jitihada zake za kubuni serikali ya umoja tangu wakati huo zimeshindwa.
Usalama umekuwa changamoto kubwa kufuatia wiki kadha za mapigano na wanamgambo wa kikurdi pamoja na mashambulizi ya bomu yanayoaminiwa kuendeshwa na kundi la Islamic State.
Rais Erdogan ameahidi kurejesha utulivu ikiwa chama chake kitapata ushindi.
No comments:
Post a Comment