Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Bwana Zidikheri Mundeme akisalimiana na wadu wa pamba baada ya kumaliza hotuba yake ilyohusu mikakati ya kuimarisha kilimo cha pamba hapa nchini.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Bwana Zidikheri Mundeme akisalimiana na wadu wa pamba baada ya kumaliza hotuba yake ilyohusu mikakati ya kuimarisha kilimo cha pamba hapa nchini.
Na Mwandishi wetu
NIBU Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Bwana Zidikheri Mundeme amewataka wadau wa zao la pamba kuwalinda wakulima wadogo wa zao
hilo kwa kuwapatia mbegu bora na madawa
sahihi ili kuboresha zao hilo.
Akiongea wakati wa
ufunguzi wa mkutano wa wadau wa zao hilo kutoka Kenya, Brazili na vituo
mbalimbali vya utafiti vya hapa nchini uliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya
White sand hivi karibuni,Bwana Mundeme amesema kutokana na mabadiliko ya hali
ya hewa nguvu za ziada zinahitajika
katika kumsaidia mkulima mdogo wa pamba hapa Tanzania.
"Kilimo cha mkataba,ukosefu wa soko na uongezaji wa
thamani na kipato kidogo cha wakulima wa zao hilo ni baadhi ya changamoto
zinazomkabili mkulima mdogo wa pamba
ambapo mkutano huu unatakiwa kuzitafutia
utatuzi changamoto hizo" aliongeza Bwana Mundeme.
Aidha amevipongeza vituo vya utafiti vya Kanda ya Ziwa kikiwemo
kituo cha utafiti Ukiriguru ambacho kilitafiti mbegu mpya ya pamba aina ya UKM 08 ambayo imekuwa ikifanya vizuri
sana kwa wakulima.

No comments:
Post a Comment