TANGAZO


Thursday, July 2, 2015

Rais Jakaya Kikwete: Tutaendelea kupambana na Malaria na kubaki kuwa historia nchini.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiongea wakati wa hafla ya uzinduzi wa kiwanda cha kuzalisha viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza malaria kilichogharimu kiasi cha bilioni 61.5 za kitanzania, ambapo alipongeza mradi huo kwani utasaidia kuondoa ugonjwa wa malaria nchini, pia aliipongeza sekta ya afya kwa kusaidia kupunguza vifo vinavyotokana na malaria kwa asilimia 71 na wagonjwa wenye kuugua malaria kwa asilimia 51 kwa kipindi cha mwaka 2004-2014 leo Mjini Kibaha. 
Waziri Mkuu wa Ethiopia na Mwenyekiti wa Viongozi wa Afrika katika Mapambano dhidi ya Malaria Mh.Hailemariam Dessalegn akiongea wakati wa hafla ya uzinduzi wa kiwanda cha kuzalisha viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza malaria ambapo aliipongeza serikali ya Tanzania katika kutekeleza Mradi huo utakaosaidia katika kupambana na vita dhidi ya malaria nchini Tanzania na Afrika kwa Ujumla, leo Mjini Kibaha. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Maendeleo laTaifa (NDC) Dkt. Chrisant Mzindakaya akiongea wakati wa hafla ya uzinduzi wa kiwanda cha kuzalisha viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza malaria na kupongeza jitihada za Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete  katika kusimamia utekelezaji wa kiwanda hicho cha kuzalisha viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza malaria ili kutekeleza ahadi yake ya kutokomeza malaria nchini, leo Mjini Kibaha. 
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo akiongea wakati wa hafla ya uzinduzi wa kiwanda cha kuzalisha viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza malaria ambapo alishukuru na kupongeza uzinduzi wa kiwanda hicho kwani kitakuwa ni mwarobaini katika mapambano dhidi ya malaria kwa mkoa wa pwani na afrika kwa ujumla,leo Mjini Kibaha. 
Waziri wa Viwanda na Biashara Mh. Abdalah Kigoda akiongea katika hafla ya uzinduzi wa kiwanda cha kuzalisha viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza malaria na kuahidi kushirikiana kwa karibu na shirika la maendeleo ya taifa (NDC) katika kutekeleza majukumu ya kiwanda hicho ili kutekeleza agizo la Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete katika vita dhidi ya malaria kupitia Mradi huo, leo Mkoani Pwani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi zawadi Waziri Mkuu wa Ethiopia na Mwenyekiti wa Viongozi wa Afrika katika Mapambano dhidi ya Malaria Mh.Hailemariam Dessalegn wakati wa hafla ya uzinduzi wa kiwanda cha kuzalisha viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza malaria leo mkoani Pwani. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Maendeleo laTaifa (NDC) Dkt. Chrisant Mzindakaya akimkabidhi zawadi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa hafla ya uzinduzi wa kiwanda cha kuzalisha viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza malaria leo mkoani Pwani. 
Waziri Mkuu wa Ethiopia na Mwenyekiti wa Viongozi wa Afrika katika Mapambano dhidi ya Malaria Mh. Hailemariam Dessalegn na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakifungua jiwe la msingi wakati wa hafla ya uzinduzi wa kiwanda cha kuzalisha viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza malaria leo mkoani Pwani. 
Waziri Mkuu wa Ethiopia na Mwenyekiti wa Viongozi wa Afrika katika Mapambano dhidi ya Malaria Mh.Hailemariam Dessalegn na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa kiwanda cha kuzalisha viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza malaria, leo mkoani Pwani. 
Waziri Mkuu wa Ethiopia na Mwenyekiti wa Viongozi wa Afrika katika Mapambano dhidi ya Malaria Mh. Hailemariam Dessalegn na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo, leo mkoani Pwani. 
Waziri Mkuu wa Ethiopia na Mwenyekiti wa Viongozi wa Afrika katika Mapambano dhidi ya Malaria Mh. Hailemariam Dessalegn akisalimiana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda wakati wa Halfa ya uzinduzi wa kiwanda cha kuzalisha viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza malaria, leo mkoani Pwani, Kushoto ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete. 
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Maendeleo laTaifa (NDC) Dkt. Chrisant Mzindakaya wakati wa Halfa ya uzinduzi wa kiwanda cha kuzalisha viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza malaria, leo mkoani Pwani,katikati ni Waziri wa Viwanda na Biashara Mh. Abdalah Kigoda.
Balozi wa Cuba nchini Tanzania Bw. Jorge Luis Lopez akiongea wakati wa hafla ya uzinduzi wa kiwanda cha kuzalisha viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza malaria kilichojengwa kwa ushirikiano wa serikali ya Cuba na Tanzania, ambapo aliahidi kuendelea kushirikiana na Serikali katika masuala balimbali ya maendeleo leo mkoani Pwani. (Picha zote na Hassan Silayo-Maelezo)

Na Benedict Liwenga-Maelezo
02/07/2015
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amefurahishwa na uzinduzi wa Kiwanda cha kuzalisha viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza ugonjwa wa malaria kilichopo eneo la viwanda, Tamco-Kibaha mkoani Pwani ikiwa ni moja ya mikakati ya Serikali iliyojipangia ya kupambana na kupunguza vifo visababishwavyo na ugonjwa huo.

Uzinduzi huo ulifanywa na mgeni rasmi ambaye ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Ethiopia, Mhe. Hailemariam Desalegn ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Nchi zinazopambana na Malaria (ALMA).

Katika uzinduzi huo, Rais Kikwete ameishukuru nchi ya Cuba kwani wao ndiyo walikubali kutoa wataalamu pamoja na teknolojia ili kuisaidia Tanzania kuendeleza sekta ya madawa ikiwemo kupambana dhidi ya ugonjwa wa malaria pamoja na kuwafundisha wataalamu wa Tanzania ili waweze kuendeleza kiwanda hicho.

Rais Kikwete alieleza kwamba, akiwa nchini Cuba mnamo Novemba 2009 alitembelea viwanda vya kuzalisha bidhaa mbalimbali za kibaiolojia kikiwemo kiwanda cha Biolarvicides cha LABIOFAM SA kinachomilikiwa na Serikali ya Cuba hivyo Serikali hiyo ilipokubali awamu ya kwanza ilipanga kujenga kiwanda cha Biolarvicides kwa lengo la kuua viluwiluwi wa mbu wanaoeneza malaria ambapo mradi huo ndo umezinduliwa rasmi tarehe 2 Julai mwaka huu na pia katika awamu ya pili ilikuwa ni ujenzi wa viwanda vya kuzalisha dawa mbalimbali kwa ajili ya kutibu na kuzuia magonjwa ya binadamu na wanyama na mwisho ni awamu ya tatu ya ujenzi wa viwanda vya dawa na vyakula vya ziada yaani Food supplement kwa ajili ya watu wenye magonjwa ya kudumu na kuzalisha mbolea za kibaiolojia (bio-fertilizers).

"Chimbuka la ujenzi wa kiwanda hiki ni ziara yangu niliyoifanya nchini Cuba, ndipo niliona kuna umuhimu wa kuiomba Serikali ya Cuba itusaidie kutupatia teknolojia pamoja na wataalamu lakini pia niliagiza Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) wajenge ushirikiano kwa ajili ya kutengeneza kiwanda nchini Kwetu na matokeo yake ndo haya", alisema Dkt. Kikwete.

Rais Kikwete alimshukuru Balozi wa Cuba nchini Tanzania, Balozi Jorge Luis Lopez kwa ushirikiano mkubwa aliouonyesha kwa kuisaidia Tanzania katika kuhakikisha kwamba kiwanda hicho kinawepo nchini na kwa ukarimu wao pasipo tamaa ya kutoa teknolojia hiyo, licha ya nchi yao kutakuwa tajiri wao walitupati teknolojia hii na walishirikiana nasi katika ujenzi wa kiwanda hicho pamoja na wataalamu

"Huu ndiyo urafiki wa kweli na udugu nakuomba Balozi unifikishie salamu zangu za dhati na shukurani zangu mimi pamoja na watanzania wote kwa ajumla kwa Rais Raul Castro kwa mchango wake mkubwa kwa nchi yetu Tanzania", Alisema Dkt. kikwete.

Naye Balozi wa Cuba nchini Tanzania, Balozi Jorge Luis Lopez ameziomba nchini nyingine ziweze kuiga ushirikiano mkubwa wa Serikali ya Tanzania na Cuba na pia kwa niaba ya Serikali yake amemshukuru Rais Kikwete kwa utendaji kazi wake mzuri, uhusiano mzuri ambao ameujenga na kati ya Tanzania na Cuba.
Naye mgeni rasmi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Ethiopia na Mwenyekiti wa Umoja wa Nchi zinazopambana na Malaria (ALMA) na ametoa pongezi zake za dhati na kueleza kwamba, hiyo ni hatua nzuri na kusema kuwa kushuka kwa idadi ya vifo nchini Tanzania ni ishara ya uongozi mzuri na bora wa Rais Kikwete na ishara nzuri kwa kuiacha nzuri katika mahali pazuri pamoja mahali pazuri dhidi ya umaskini

Aidha, ameeleza kuwa uwepo wa kiwanda hiko itakuwa ni ishara nzuri ya mapambano na yeye kama Mwenyekiti wa Umoja wa nchi zinazopambana (ALMA) dhidi ya malaria atazihamasisha nchi nyingine kutumia Afrika waweze kutumia mazao yatokanayo na kiwanda hicho.

Kampuni ya Tanzania Biotech Products Limited ni Kampuni iliyoundwa kwa ajili ya kuendesha Kiwanda cha kuzalisha Viuadudu vya kuua Viluwiluwi vya mbu wanaoeneza malaria kilichopo Kibaha, Pwani ambacho kimejengwa kwa kushirikiana na Kampuni ya LABIOFAM SA ya Cuba a kiwanda hiki kinatokana na agizo l Rais Kikwete alilolito Januari 4 , 2010 kwa shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) baada ya ziara yake nchini Cuba.

No comments:

Post a Comment