TANGAZO


Tuesday, June 23, 2015

Ziara ya Kinana Sengerema-Misungwi

Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akikagua hali ya Soko Kuu la Halmashauri ya mji wa Sengerema, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM na uhai wa Chama mkoani Mwanza leo. Soko hilo limelalamikiwa na watumiaji kuwa na uchafu uliokithiri katika maeneo mbalimbali vikiwemo vyoo.
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akikagua ujenzi tangi na chujio la maji la  mradi wa maji wa Sengerema mjini uliopo eneo la Nyamazugowa, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM na uhai wa Chama mkoani Mwanza.
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akikata utepe kuzindua Kivuko Super Sumar kinachofanya kazi ya kusafirisha abiria, mizigo, na magari kutoka Bandari ya Kamanda, Sengerema hadi Mwanza. Kivuko hicho kina uwezo wa kubeba abiria 300 na magari kati ya 20 a 50 kuuatana na ukubwa.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia maelfu ya wananchi waliojitokeza katika mkutano wa hadhara aliofanya katika viwanja vya Ofisi ya CCM, wilaya ya Sengerema mjini, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM na Uhai wa Chama mkoani Mwanza leo.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akiwa na baadhi ta viongozi wa chama hicho akishuka kwenye kivuko MV Misungwi, alipowasili wilayani Misungwi kuanza ziara ya kikazi.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akiangalia ngoma ya utamaduni wakati wa mapokezi eneo la Usagara, alipowasili  wilayani Misungwi, Mwanza,  kuanza ziara ya kikazi jana, akitokea Jimo la Sengerema. (Picha zote na Richard Mwaikenda)

No comments:

Post a Comment