TANGAZO


Thursday, June 25, 2015

Tanzania yatoa elimu ya Uendeshaji na Usimamiaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana kwa ujumbe kutoka Zimbabwe

Kaimu Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Barnabas Ndunguru akifungua mkutano kati ya maafisa Vijana kutoka Wizara hiyo na ujumbe kutoka Nchi ya Zimbabwe waliofika Wizarani hapo jana jijini Dar es Salaam kujifunza namna Wizara inavyosimamia uendeshaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana.
Kaimu Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Venerosa Mtenga (kulia) akizungumza na ujumbe kutoka Nchi ya Zimbabwe waliofika katika ofisi za Wizara hiyo jana jijini Dar es Salaam kujifunza namna Wizara inavyosimamia uendeshaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana. Kushoro ni Kaimu Mkurugenzi wa uwezeshaji uchumi kutoka Wizara ya Vijana, na uwezeshaji Uchumi nchini Zimbabwe Bw. Tafi Greemas Mashonganyika.
Kaimu Mkurugenzi wa uwezeshaji uchumi kutoka Wizara ya Vijana, na uwezeshaji Uchumi nchini Zimbabwe Bw. Tafi Greemas Mashonganyika (aliyesimama) akielezea lengo la ujio wake na wajumbe kadhaa nchini Tanzania baada ya kukutana na maafisa vijana wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo jana jijini Dar es Salaam. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana Bibi. Venerosa Mtenga na Kulia ni Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Barnabas Ndunguru.
Ofisa Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Eliakim Mtawa akitoa mada ya uendeshaji na usimamizi wa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana kwa ujumbe kutoka nchini Zimbabwe waliofika Tanzania kujifunza juu ya Mfuko huo jana Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Fedha na Utawala kutoka Wizara ya Vijana, na uwezeshaji Uchumi nchini Zimbabwe Bw. Emmanuel Ngwarati (mwenye miwani) akichangia mada wakati wa mkutano kati ya maafisa Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na ujumbe kutoka Nchi ya Zimbabwe waliofika Wizarani hapo jana jijini Dar es Salaam kujifunza namna Wizara inavyosimamia uendeshaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa uwezeshaji uchumi kutoka Wizara ya Vijana, na uwezeshaji Uchumi nchini Zimbabwe Bw. Tafi Greemas Mashonganyika. 
Maofisa Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo pamoja na ujumbe kutoka Wizara ya Vijana na uwezeshaji Uchumi nchini Zimbabwe wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizokua zikiendelea wakati wa ziara ya kujifunza juu ya uendeshaji na usimamizi wa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana nchini Tanzania.
Ofisa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Vijana na uwezeshaji Uchumi nchini Zimbabwe Bi. Klery Chikwede (aliyepiga magoti) akimkabidhi Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Barnabas Ndunguru (kulia) zawadi kama shukrani kwa Wizara kukubali kuwapokea na kuwapa elimu ya uendeshaji na usimamizi wa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi Maendeleo ya Michezo Bibi. Venerosa Mtenga.  
Kaimu Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana Bibi. Venerosa Mtenga katika picha ya pamoja ya Maofisa Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo pamoja na ujumbe kutoka Wizara ya Vijana na uwezeshaji Uchumi nchini Zimbabwe wakati wa ziara ya ujumbe huo nchini Tanzania kujifunza juu ya uendeshaji na usimamizi wa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana.

No comments:

Post a Comment