TANGAZO


Wednesday, June 24, 2015

Mlipuko wawaua watu 12 Mogadishu


Mogadishu Somalia

Mlipuaji wa kujitolea muhanga ameligongesha gari lake na lile la kijeshi katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu na kusababisha mlipuko mkubwa.
Ripoti zinasema kwamba takriban watu 12 waliuawa na wengine kujeruhiwa wengi wakiwa raia.
Shambulizi hilo lilitokea karibu na ubalozi wa falme za kiarabu UAE
Vyombo vya habari nchini Somalia vimeripoti kwamba balozi amenusurika mlipuko huo ambao umeutaja kama jaribio la mauaji.

No comments:

Post a Comment