TANGAZO


Monday, June 29, 2015

Kiongozi wa mashtaka nchini Misri afariki

Hisham Barakat afariki
Kiongozi wa mashtaka nchini Misri Hisham Barakat amefariki kutokana na majeraha aliopata baada ya bomu kulipua gari lake mjini Cairo.
Msafara wa Bwana Barakat ulishambuliwa ulipokuwa ukipitia katika wilaya ya Heliopolis.
Nguvu za shambulio hilo ziliharibu baadhi ya nyumba na maduka.Walinzi wawili wa bwana Barakat pia walijeruhiwa.
null
Bomu lalipua gari la Hisham Barakat
Bwana Barakat amekuwa akipendekeza mamia ya wapiganaji hao kufunguliwa mashtaka tangu kupinduliwa kwa rais aliyepinduliwa , Mohamed Morsi, mwaka 2013.
Kundi linalojiita Popular Restistance of Giza limekiri kutekeleza shambulizi hilo.

No comments:

Post a Comment