TANGAZO


Monday, May 4, 2015

Kikao cha SMT na SMZ kutatua kero za Muungano chafanyika Zanzibar

Waziri wa Fedha  Mhe. Saada Salum Mkuya  na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha  na Mlipaji Mkuu wa Serikali  Dr. Servacius Likwelile wakiwa kwenye kikao kilichofanyika Dar es salaam pamoja  na viongozi wa Hazina (hawapo kwenye picha) siku moja kabla ya kwenda Zanzibar. 
Waziri wa Fedha  Mhe. Saada Salum Mkuya  akifafanua jambo linalohusu kero ya Muungano  kikao kilichofanyika mjini Dar es salaam kati yake na viongozi wa Hazina siku moja kabla ya kwenda Zanzibar. 
Waziri wa Fedha  Mhe. Saada Salum Mkuya akisalimiana na Mhe. Omar Y. Mzee Waziri wa Fedha Zanzibar mara baada ya kuwasili Zanzibar kwa ajili ya mazungumzo kuhusu kutatua kero za Muungano hapa Zanzibar.
Waziri wa Fedha  Mhe. Saada Salum Mkuya  na Mhe. Omar Y. Mzee Waziri wa Fedha Zanzibar  wakibadilishana mawazo kabla kikao cha kuzungumzia utatuzi wa kero za Muungano hazijaanza. Wa katikati aliyevaa miwani ni Bw. Rished Bade Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya mapato Tanzania.
Waziri wa Fedha  Mhe. Saada Salum Mkuya akiwa na Prof. Adolf Mkenda Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha wa kulia, pamoja na Bw. Rished Bade Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya mapato Tanzania, wakishauriana jambo kabla ya kuanza kwa kikao cha utatuzi wa kero za Muungano Zanzibar. 
Waziri wa Fedha Zanzibar, Mhe. Omar  Y. Mzee Waziri akisisitiza jambo kwa ujumbe kutoka SMT na SMZ katika kikao cha kutatua kero za Muungano kilichofanyika leo mjini Zanzibar. Kutoka kushoto kwa SMZ ni Bw. Mwita Mgeni Kamishna wa Bajeti – Wizara ya Fedha ZNZ, Bw.Abdi Fakih Kamishna- ZRB, Mhe. Omar Y. Mzee Waziri wa Fedha – ZNZ na  Bw. Juma Ameir , Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha- ZNZ.
Waziri wa Fedha  Mhe. Saada Salum Mkuya akionyesha kwa wajumbe kutoka SMT na SMZ mfano wa kero ambayo inatakiwa kufanyiwa kazi mara moja katika kikao maalum kilichofanyika Zanzibar kwa madhumuni ya kutatua kero hizo. 
Prof. Adolf Mkenda, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha akijaribu kutetea hoja yake kwa Waziri wa Fedha Zanzibar,  Mhe. Omar Y. Mzee ( hayupo kwenye picha)katika kikao cha kutatua kero za Muungano kilichofanyika leo hapa Zanzibar. (Picha zote na Ingiahedi  Mduma na Scola Malinga – Zanzibar)

No comments:

Post a Comment