Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete (kulia), akipata maelezo kutoka kwa Msimamizi wa ujenzi kutoka Kambi ya Mzinga ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Aloyce Mayunga (kushoto), alipokwenda kukagua ujenzi wa maabara ya Shule ya Sekondari ya Kiwangwa wakati wa ziara ya kikazi katika Kata ya Kiwangwa, wilayani Chalinze, mkoani Pwani jana. Aliwataka wajenzi hao kujenga maabara hayo kwa kuzingatia viwango. Katikati ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Bagamoyo, Saleh Mpimbwi.
Ridhiwani Kikwete akizungumza na wakandarasi kutoka Kambi ya Mzinga ya JWTZ wanaojenga maabara ya Shule ya Sekondari ya Kiwangwa wakati wa ziara ya kuagua miradi ya maendeleo na kuwashukuru wananchi kwa kumchagua kuwa mbunge miezi sita iliyopita. (Picha zote na Richard Mwaikenda wa Kamanda wa Matukio Blog) 
Ridhiwani akinyoosha juu kadi ya Chadema aliyokabidhiwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Kijiji cha Masugulu ambaye amehamia CCM katika mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Mwitemo Kata ya Kiwangwa jana. Mbunge Ridhiwani akihutubia wananchi katika Kijiji cha Mwitemo jana. Sehemu ya akina mama wakisikiliza kwa makini wakati Ridhiwani Kikwete akihutubia katika Kitongoji cha Magogoni, Kijiji cha Msinune, Kata ya Kiwangwa. Ridhiwani Kikwete akihutubia wananchi katika Kijiji cha Msinune, Kata ya Kiwangwa. Msanii kiongozi wa Kikundi cha sanaa cha Chanzala akifanya maajabu yake wakati mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Mbunge Ridhiwani Kikwete katika Kata ya Kiwangwa jana. Msanii kiongozi wa Kikundi cha sanaa cha Chanzala akifanya manjonjo yake wakati wa mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Mbunge Ridhiwani Kikwete, Kiwangwa jana.
Mwenyekiti mpya wa Serikali ya Kijiji cha Kiwangwa, Kata ya Kiwangwa, akifungua rasmi mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete katika Kata ya Kiwangwa ambapo pamoja na kusikiliza kero zao aliwashukuru wananchi kwa kumchagua mwaka jana. Mmoja wa wakazi wa Kiwangwa akizungumza katika mkutano huo jana. Mkazi wa Kiwangwa Shabani Dume akiuliza swali kwa kumtaka Mbunge Ridhiwani asaidie kuwepo dampo katika Kijiji cha Kiwangwa jana. Kassim Makelele wa Kata ya Kiwangwa akimuomba Mbunge Ridhiwani kununua Ambulance kwa ajili ya Kituo cha Afya cha Kiwangwa. Diwani wa Viti Maalumu Tarafa ya Msata, Rehema Mno akielezea kwa wananchi jinsi alivyoshiriki kutatua kero za wananchi katika Kata ya Kiwangwa. Ridhiwani akiteta jambo na Diwani wa Kata ya Kiwangwa, Yahaya Ramadhani wakati wa mkutano huo. Sehemu ya umati uliohudhuria katika mkutano huo. Ridhiwani akihutubia katika mkutano huo ambapo aliwaambia viongozi wa Tanesco kuhakikisha wana peleka haraka umeme wa Wakala wa Umeme Vijijini (REA) katika Kijiji cha Kiwangwa. Meneja wa Tanesco Wilaya ya Chalinze, Julius Doyi akiwaambia wananchi wa Kiwangwa kuwa umeme utaingia hapo mwezi huu. Meneja wa Mamlaka ya Maji Safi na Taka wa Chalinze, Injinia Christer Mchomba, akielezea kwa wananchi mikakati mbalimbali ya kuharakisha upatikanaji wa maji katika Kata ya Kiwangwa. Ridhiwani akaimkabidhi Bondia Idd Pialali gloves 20 kwa ajili ya kuendeleza mchezo wa ngumi katika Kata ya Kiwangwa. Ridhiwani akimkabidhi mpira mmoja wa wa manahodha wa timu mbalimbali katika Kata ya Kiwangwa kwa ajili ya kuendeleza soka katika kata hiyo.
Ridhiwani akinyoosha juu kadi ya Chadema aliyokabidhiwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Kijiji cha Masugulu ambaye amehamia CCM katika mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Mwitemo Kata ya Kiwangwa jana. Mbunge Ridhiwani akihutubia wananchi katika Kijiji cha Mwitemo jana. Sehemu ya akina mama wakisikiliza kwa makini wakati Ridhiwani Kikwete akihutubia katika Kitongoji cha Magogoni, Kijiji cha Msinune, Kata ya Kiwangwa. Ridhiwani Kikwete akihutubia wananchi katika Kijiji cha Msinune, Kata ya Kiwangwa. Msanii kiongozi wa Kikundi cha sanaa cha Chanzala akifanya maajabu yake wakati mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Mbunge Ridhiwani Kikwete katika Kata ya Kiwangwa jana. Msanii kiongozi wa Kikundi cha sanaa cha Chanzala akifanya manjonjo yake wakati wa mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Mbunge Ridhiwani Kikwete, Kiwangwa jana.
Mwenyekiti mpya wa Serikali ya Kijiji cha Kiwangwa, Kata ya Kiwangwa, akifungua rasmi mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete katika Kata ya Kiwangwa ambapo pamoja na kusikiliza kero zao aliwashukuru wananchi kwa kumchagua mwaka jana. Mmoja wa wakazi wa Kiwangwa akizungumza katika mkutano huo jana. Mkazi wa Kiwangwa Shabani Dume akiuliza swali kwa kumtaka Mbunge Ridhiwani asaidie kuwepo dampo katika Kijiji cha Kiwangwa jana. Kassim Makelele wa Kata ya Kiwangwa akimuomba Mbunge Ridhiwani kununua Ambulance kwa ajili ya Kituo cha Afya cha Kiwangwa. Diwani wa Viti Maalumu Tarafa ya Msata, Rehema Mno akielezea kwa wananchi jinsi alivyoshiriki kutatua kero za wananchi katika Kata ya Kiwangwa. Ridhiwani akiteta jambo na Diwani wa Kata ya Kiwangwa, Yahaya Ramadhani wakati wa mkutano huo. Sehemu ya umati uliohudhuria katika mkutano huo. Ridhiwani akihutubia katika mkutano huo ambapo aliwaambia viongozi wa Tanesco kuhakikisha wana peleka haraka umeme wa Wakala wa Umeme Vijijini (REA) katika Kijiji cha Kiwangwa. Meneja wa Tanesco Wilaya ya Chalinze, Julius Doyi akiwaambia wananchi wa Kiwangwa kuwa umeme utaingia hapo mwezi huu. Meneja wa Mamlaka ya Maji Safi na Taka wa Chalinze, Injinia Christer Mchomba, akielezea kwa wananchi mikakati mbalimbali ya kuharakisha upatikanaji wa maji katika Kata ya Kiwangwa. Ridhiwani akaimkabidhi Bondia Idd Pialali gloves 20 kwa ajili ya kuendeleza mchezo wa ngumi katika Kata ya Kiwangwa. Ridhiwani akimkabidhi mpira mmoja wa wa manahodha wa timu mbalimbali katika Kata ya Kiwangwa kwa ajili ya kuendeleza soka katika kata hiyo.

No comments:
Post a Comment