Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein.
Na Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Na Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati
wote itazingatia umuhimu wa kuwapatia wanajeshi huduma zao kwa kadiri hali ya
uchumi inavyoruhusu likiwemo suala zima la kuwapatia makaazi bora katika
makambi yao.
Rais wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein aliyasema hayo
katika hafla ya uwekaji wa jiwe la
msingi la mradi wa ujenzi wa nyumba 320 za makaazi ya Wanajeshi katika Kambi ya
Ali Khamis kisiwani Pemba, ikiwa ni miongoni mwa shamra shamra za maadhimisho
ya miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Katika hotuba
yake Dk. Shein alisema kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
inazingatia suala la umuhimu wa makaazi kwa
Wanajeshi kama ni moja ya mahitaji muhimu kama ilivyo kwa vitendea kazi
vyengine.
“Ni jambo la
kushukuru kwamba leo tumefikia hatua hii ya utekelezaji wa mradi mkubwa wa
nyumba hizo pia, napenda nikuahidini kwamba juhudi hizi hazitaishia kwenye
mradi huu kwani lengo letu ni kuona wanajeshi wetu wote wanaishi
kambini”,alisema Dk. Shein
Aidha, Dk. Shein
alisema kuwa Serikali ys ajasmhuri ya
Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zinathamini
jukumu muhimu linalotekelezwa na Jeshi la Ulinzi la Tanzania na Vikosi vyengine
vya ulizni na usalama na zote kwa pamoja
zitaendelea kuzifanyia kazi changamoto zilizopo ili kuongeza ufanisi katika
utekelezaji wa majukumu yao.
Dk. Shein alisema
kuwa ni wazi kuwa suala la watumishi wakiwemo askari kuishi katika nyumba za
kupanga lina changamoto zake na kusisitiza kuwa mradi huo ni kielelezo cha dhamira ya dhati ya Serikali
kupunguza tatizo la makaazi kwa wanajeshi wake.
Pamoja na hayo,
Dk. Shein alisema kuwa katika kipindi cha miaka 53 tangu upatikane uhuru wa
Tanzania Bara na miaka 51 tangu yafanyike Mapinduzi Matukufu ya Januari 12,
mwaka 1964, Jeshi la Wananachi wa Tanznia limeonesha uwezo mkubwa wa kiulinzi
katika mipaka ya tanzania pamoja na operesheni mbali mbali za kimataifa
ilizoshiriki.
Alisema kuwa
uwezo, umahiri na nidhamu ya Jeshi la Tanzania kunaleta faraja na kutoa taswira
njema ya ulizni wa Tanzania Kimataifa. “Kwa kweli, tunaona fahari kuwa na Jeshi
lenye uwezo na sifa kama ilivyo kwa Jeshi la Wananachi wa Tanzania”,alisema Dk.
Shein.
Dk. Shein alisema
kuwa Jeshi la Wananachi wa Tanzania litabaki kukumbukwa kutokana na mchango wake wa kusaidia wapiganaji uhuru
Kusini mwa Bara la Afrika katika mika ya 70 na katika mapambano ya kumtoa Nduli
Iddi Amin aliyeivamia Tanzania mnamo mwaka 1978.
Aidha, Dk. Shein
alitoa pongezi zake kwa Jeshi hilo kutokana na umahiri wake ambao umeendelea
kusikika huko Dafur- Sudan na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambapo lilishiriki katika operesheni za
kusimamia amani za kimataifa sambamba na kusifu mchango wake katika michezo
pamoja na kutoa huduma za afya na elimu kwa jamii.
Dk. Shein
alitumia fursa hiyo kwa kutoa shukurani kwa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China
kupitia Benki ya Exim ya China kwa kukubali kutoa mkopo uliowezesha utekelezaji
wa ujenzi wa nyumba 6,064 hapa nchini katika awamu ya kwanza ya mradi wenye
lengo la kujenga nyumba 10,000.
Alieleza kuwa
hicho ni kielelezo chengine cha uhusiano mwema na wa kihistoria uliokuwa nao
Jamhuri ya Watu wa China kwa zaidi ya miaka 50 hivi sasa ambapo pia, Dk. Shein
alitumia fursa hiyo kuwapongeza wakandarasi wa Shangai Construction Group
(General) Company ya China ambao wanaendelea kutekeleza mradi huo wa ujenzi wa
nyumba za wanajeshi.
Sambamba na hayo,
Dk. Shein alisema kuwa ni wajibu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
kutambua uzito wa jukumu kubwa liliyopo katika kuhakikisha usimamizi mzuri wa
mradi huo ili utekelezaji wake uwe na ufanisi uliokusudiwa.
Mapema Waziri wa
Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dk. Hussein Mwinyi alisema kuwa mchakato wa
mradi huo ulianza rasmi mwaka 2011 kwa mazungumzo baina ya Serikali ya Tanzania
na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na wafadhili ambapo makubaliano hayo ni
kujenga nyumba 10,000 kwa makundi yote ya wnajeshi kwa gharama ya Dola za
Kimarekani milioni 300.
Alisema kuwa
katika fedha hizo Serikali ya Tanzania inachamgia Dola milioni 15 na Dola
milioni 285 zilizobaki ni za mkopo nafuu kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu wa
China kupitia Benki ya Exim ya China.
Alisema kuwa
awamu ya kwanza ya ujezni huo imeanza kwa vikosi vilivyopo mikoa ya
Dar-es-Salaam na Pwani ambapo jumla ya nyumba 391 za familia 3,128 zinajengwa
na kuendelea kueleza kuwa ujenzi wa nyumba 145 kwa familia 1,160 zilziokuwa
zikijengwa kwenye maeneo manne ya Dar-es-Salaam umekamilika na tayari
zimeshakabidhiwa kwa Jeshi la Wananachi wa Tanzania.
Dk. Mwinyi
alisema kuwa ujenzi wa nyumba 141 zilzobaki kwa Mkoa wa Dar-es-Salaam za
familia 1,128 zikzo katika hatua ya umaliziaji na zinatarajiwa kukabidhiwa muda
wowote mwezi huu huku akieleza kuwa awamu ya pili ya ujenzi wa nyumba 329 kwa
familia 2,632 kwenye maeneo ya vikosi vilivyopo mikoa ya Arusha, Dodoma,
Morogoro, PEMBA na Tanga ilianza mnamo mwezi Oktoba mwaka jana.
Mapema Mnadhimu
Mkuu wa Jeshi la Wananachi wa Tanzania Luteni Jenerali Samuel Ndomba, alieleza
juhudi zinazoendelea katika ujenzi huo sambamba na azma ya ujenzi wa nyumba
hizo wa Wanajeshi.
No comments:
Post a Comment