TANGAZO


Saturday, January 17, 2015

Mechi za kombe la Afrika kuanza leo

Kinyanganyiroi cha kombe la Afrika kuanza leo nchini Equitorial Guinea
Timu kutoka kote Afrika zimewasili nchini Equatorial Guinea wakati ambapo mechi za taifa bingwa barani zitarajiwa kung'oa nanga hii leo ikiwa ni miezi miwili tangu taifa hilo la afrika ya kati likubali kuandaa mechi hizo.
Morocco ndiyo iliokuwa iandae kombe hilo lakini badala yake ikaomba kuahirishwa kwake kutokana na hofu ya kusambaa kwa ugonjwa wa ebola.
Shirikisho la kandanda barani Afrika CAF hata hivyo lilikataa ombi hilo la Morocco
Mkuu wa CAF (Hicham El Amrani) anasema kuwa kila tahadhari imechukuliwa nchini Equatorial Guinea kuwalinda watu kutokana na ugonjwa wa ebola.
Mechi ya kwanza itakuwa kati ya wenyeji Equatorial Guinea na Congo

No comments:

Post a Comment