TANGAZO


Friday, January 16, 2015

Bondia Muhammad Ali anaendelea vizuri

Mstaafu wa masumbwi Duniani Muhammad Ali
Hali ya afya ya gwiji wa zamani wa ndondi Duniani Muhammad Ali inaendelea vizuri
Bondia huyo alirudishwa hospital kwa tatizo la maradhi ya maambukizi ya njia ya mkojo.
Msemaji wa familia Bob Gunnell alisema "Ali yuko imara na anatarajiwa kutolewa leo,kulikua na uchunguzi zaidi juu ya maambukizi yake.
Ali mwenye miaka 72 kabla alitolewa hospitali mapema mwezi huu baada ya kupatiwa mabaibatu kwa wiki mbili kwa maradhi yanayomsumbua.
Bondia huyo aliwahi kuwa bigwa wa dunia kwa uzito wa juu alistaafu mchezo huo mwaka 1981.

No comments:

Post a Comment