TANGAZO


Thursday, December 4, 2014

Dk. Shein akutana na Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani wa Wilaya ya Mkoani Pemba

Ustadhi Mohamed Juma Issa (kushoto) akisalimiana na  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein  baada ya kusoma Quran Tukufu wakati wa  Mkutano wa Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani za CCM Wilaya ya Mkoani  leo   katika ukumbi wa Chuo cha Fidel Castro  akimalizia ziara za kuimarisha Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kusini Pemba. (Picha zote na Ikulu)
Sheikh Abdalla Yussuf Ali alipokuwa akitoa tafsiri ya Quran iliyosomwa na Sheikh Mohammed Juma Issa (hayupo pichani) katika kufungua Mkutano wa Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani za CCM Wilaya ya Mkoani  uliohutubiwa  na  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein  katika ukumbi wa Chuo cha Fidel Castro  leo akimalizia ziara za kuimarisha Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kusini Pemba. 
Wasoma Utenzi Saada Mohamed Zahran na Asha Mohamed Ng’wali wakihani utenzi wao katika wa  Mkutano wa Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani za CCM Wilaya ya Mkoani leo uliofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Fidel Castro  chini ya Mwenyekiti wake  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein akimalizia ziara za kuimarisha Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kusini Pemba.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mkoani Omar Makame Haji akimakaribisha Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai wakati wa Mkutano wa Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani za CCM Wilaya ya Mkoani uliofanyika leo katika ukumbi wa Fidel Castro chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein  akimalizia ziara zake za kuimarisha Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kusini Pemba.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein  akipokea risala kutoka kwa msomaji Mwanajuma  Hassan Kaduara katika wa Mkutano wa Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani za CCM Wilaya ya Mkoani uliofanyika leo katika ukumbi wa Fidel Castro akimalizia ziara zake za kuimarisha Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kusini Pemba.
Baadhi ya wajumbe wa Mkutano wa Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani za CCM Wilaya ya Mkoani   wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein alipozungumza nao leo katika ukumbi wa Chuo cha Fidel Castro akiwa katika umaliziaji wa ziara za kuimarisha Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kusini Pemba.
Baadhi ya Viongozi na Wazee wa Chama cha Mapinduzi CCM na wajumbe wa Mkutano wa Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani za CCM Wilaya ya Mkoani  wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein alipozungumza nao leo katika ukumbi wa Chuo cha Fidel Castro akimalizia ziara za kuimarisha Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kusini Pemba.
Balozi kutoka Jimbo la Makoong’we Bi. Salama Bakari  ni  miongoni mwa Mabalozi waliotoa michango mbali mbali katika Mkutano wa Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani  wa Wilaya ya Mkoani uliofanyika leo katika ukumbi wa Chuo cha Fidel Castro na kuhutubiwa na  Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohasmed Shein.
Balozi kutoka Jimbo la Makoong’we Bi. Asma Abdalla Abdii ni  miongoni mwa Mabalozi waliotoa michango mbali mbali katika Mkutano wa Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani  wa Wilaya ya Mkoani uliofanyika leo katika ukumbi wa Chuo cha Fidel Castro na kuhutubiwa na  Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali MOhasmed Shein.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein  pia Makamo Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar alipokuwa akitoa hutuba yake leo kwa kuzungumza na  Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani za CCM wa Wilaya ya Chake chake Mkoa wa Kusini Pemba akiwa katika ziara za kuimarisha chama.

Na Ramadhan Othman, Pemba
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ameitahadharisha jamii dhidi ya vitendo vya ubaguzi, bugudha na manyanyaso kwa misingi ya kisiasa na kueleza kuwa vitendo hivyo vinaiangamiza jamii.
Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Maziwang’ombe katika wilaya ya Micheweni Mkoa Kaskazini Pemba jana, Dk. Shein alisema wananchi ni lazima wazingatie sheria ya kuanzishwa vyama vingi ambayo imeeleza wazi kuwa kila mwananchi ana haki na uhuru wa kujiunga na chama chochote cha siasa na kushiriki siasa bila kubaguliwa.
“tusiwarithishe chuki wala ugomvi watoto wetu kwani tukiendelea kufanya hivyo tutakuwa tunaiangamiza jamii yetu ambayo tangu Mapinduzi ya mwaka 1964 ilikuwa ikiishi kwa amani na upendo” Dk. Shein alisema.
Aliwaeleza wananchi hao kuwa tofauti za itikadi za kisiasa isiwe kisingizio cha kufanyiana chuki, kubaguana na kubugudhiana au kutengana kwani watu wote ni ndugu na wanahitaji kuishi pamoja kwa upendo na kusaidiana.
“Mzazi atabaki kuwa mzazi, mtoto atabaki kuwa mtoto, ndugu atabaki kuwa ndugu; inakuwaje tunafanyiana visa na kuhasimiana kwa kuwa tu mwenzetu mmoja ametoka chama hiki kwenda chama kingine?” aliuliza Dk. Shein.
Dk. Shein ambaye alifika kijijini hapo kukabidhi boti na mashine ya kisasa yenye injini ya uwezo wa nguvufarasi 40 kwa kikundi cha Heri ya Moyo Mmoja ambacho ni vijana waliohama chama cha CUF na kujiunga na CCM. 
Vijana hao walifanyiwa visa vya kunyimwa huduma muhimu na hata kuondolewa katika kazi za pamoja ikiwemo kutengwa katika shughuli za ushirika ndani ya kijiji hicho.
“kwa nini wanaotoka katika chama muwabaguwe, muwanyime riziki kwa kuwaondoa katika ushirika wakati hao ni ndugu zenu na si mahasimu wenu? Mnafanya hivyo kutokana na siasa za chuki hivyo si sivyo” Dk. Shein aliwaeleza wananchi hao.

Alifafanua kuwa  watu wa Maziwang’ombe hawakuwa na tabia hiyo na wamekuwa wakiishi kwa upendo katika maisha yao yote kwa kuheshimiana lakini iweje tangu mfumo wa vyama vingi uliporejeshwa mwaka 1992 wajenga chuki kati yao.
Aliwakumbusha kuwa vyama vya siasa vinakuja na kupita hivyo hawana budi kuzingatia maisha yao na kuishi kwa amani na maelewano kama ambavyo viongozi wao wanavyoishi na kufanya kazi kwa pamoja.
“Mimi na Maalim Seif hatugombani, hatutukanani. Sijagombana naye wala Mawaziri wanaotoka katika chama cha CUF, wananiheshimu nami nawaheshimu, tunaheshimiana na sote tunatekeleza maagizo ya serikali” Dk. Shein aliwaambia wananchi hao akimaanisha kuwa viongozi hao wanatekeleza majukumu yao katika Baraza la Mapinduzi bila kuonesha tofauti yeyote.
Aliwaeleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar iliyo chini ya Mfumo wa Umoja wa Kitaifa haibagui na ndio kiini cha mafanikio iliyoyapata hadi sasa.
“Tunahudumia wananchi wote bila ya kuangalia itikadi ya mtu na kama tungefanya ubaguzi tusingefika hapa tulipo” alisema na kuwaeleza watu wa Maziwang’ombe kuwa “ kubaguana si uhodari”.
Aliwataka wananchi hao kuendelea kushiriki katika shughuli za maendeleo ili kujenga uchumi wa taifa kwa kufanya kazi kwa bidii na kuwahakikishia kuwa serikali itaendelea kushughulikia masuala mengine muhimu ya kuendeleza nchi ikiwemo kuimarisha miundombinu ya bara bara, skuli, hospitali, maji safi na salama, umeme na mambo mengine makubwa kwa lengo la kuimarisha huduma za jamii.
Hata hivyo, aliwaasa kutosita kuchangia baadhi ya gharama wanazotakiwa kutoa wakati wakipata baadhi ya huduma ikiwemo ununuzi wa madaftari kwa watoto wao wanaokwenda skuli, kutokana na ukweli kwamba idadi ya watu imekuwa ikiongezeka kwa kasi kubwa kuliko uwezo wa serikali kuweza kumudu mahitaji yao.
Alisisitiza kuwa hivi sasa serikali haina uwezo tena wa kutoa ajira kwa kila mwananchi na kuwahimiza kuanzisha vikundi ili serikali iwasaidie na kubainisha kuwa serikali imedhamiria kuhakikisha kuwa wananchi wanaojikusanya katika vikundi vya uzalishaji na ushirika wanapatiwa misaada itakayowezesha shughuli za kuwa endelevu.
“Tupo hapa kutekeleza ahadi yetu na kusaidia wananchi wenzetu, undeni vikundi vya kujiajiri, kama mtaendelea kujiunga katika vikundi tutazidi kuwasaidia” Dk. Shein alisisitiza. 
Katika mkutano huo uliohudhuriwa na mamia ya wananchi wa kijiji hicho na vijiji vya jirani, Dk. Shein aliwakumbusha wananchi kuzingatia historia yao na kuwahimiza kudumisha amani na utulivu na kuwatahadharisha dhidi ya kushiriri katika vitendo vya uvunjifu wa amani kwa kuwa vyombo vinavyohusika na ulinzi na usalama havitawavumilia.   
Wakati huo huo Waziri wa Ustawi wa Jamii, Uwezeshaji, Vijana, Wanawake na Watoto Bi Zainab Mohamed Omar aliwahimiza wananchi kujiunga katika vikundi kama walivyofanya wana kikundi cha Heri ya Moyo Mmoja ili waweze kufaidika na mpango wa Serikali wa kuwawezesha wananchi kiuchumi ambao uko chini ya Wizara yake.
Mpango huo wa kuwawezesha wananchi kiuchumi umelenga kuongeza ajira kwa wananchi kujiajiri wenyewe kwa kuwa mazingira ya sasa hayaruhusu kila mwananchi kupata kazi za kuajiriwa serikalini. 
Kikundi hicho kinajumuisha vijana waliokihama Chama cha wananchi (CUF) na kuhamia Chama cha Mapinduzi (CCM) uamuzi ambao uliwafanya kunyimwa baadhi ya huduma muhimu kijijini kwao.
Kwa upande wake Naibu Katibu Mku wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai alihimiza wananchi kufanya siasa bila ya kubugudhiana au kuwekeana visasi kwa kuwa wakati huo umepita na kuwataka kufuata nyayo za viongozi wakuu wa vyama vyao ambao wanafanyakazi pamoja bila ya mivutano.
“viongozi wetu wakuu wanafanyakazi kwa maelewano makubwa bila mivutano…nasi tufanye hivyo hivyo tusilete chuki miongoni mwetu na kuumizana na serikali inaonesha mfano kwa kuleta huduma kwa wananchi bila ya kubagua” alisema Naibu Katibu Mkuu huyo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi anatarajiwa kumaliza ziara yake ya siku nne kisiwani humu kwa kuzungumza na viongozi wa mashina na wenyeviti wa maskani za CCM wa Wilaya ya Mkoani, mkoa wa Kusini Pemba.

No comments:

Post a Comment