TANGAZO


Friday, November 14, 2014

Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) afanya ziara kwenye vitengo vya Mawasiliano Serikalini



Katibu, Ofisi ya Rais Sekretariet ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Exavier Daudi (kushoto) akimkaribisha ofisini kwake Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene wakati alipotembelea ofisi hiyo kwa lengo la kuangalia utendaji kazi wa kitengo cha mawasiliano.


Katibu, Ofisi ya Rais Sekretariet ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Exavier Daudi akimueleza Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene kuhusu mikakati ya ofisi hiyo ya kuboresha mawasiliano ya serikali kwa umma wakati wa ziara ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari katika vitengo cha mawasiliano.


Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene (kushoto) akizungumza na Katibu, Ofisi ya Rais Sekretariet ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Exavier Daudi wakati alipotembelea ofisi hiyo ikiwa ni utekelezaji wa mkakati wa Idara ya Habari kutembelea vitengo vya mawasiliano kwenye taasisi za serikali ili kuangalia utendaji kazi wa vitengo hivyo.


Ofisa Habari wa Ofisi ya Rais Sekretariet ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Kassim Nyaki (kulia) akieleza kwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene kuhusu mafanikio ya kitengo cha mawasiliano cha ofisi hiyo  katika kutoa taarifa kwa umma ambapo alisema hadi sasa tovuti yao ina zaidi ya watu Elfu 8 wanaotembelea kwa siku.


Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene (kulia mwenye Kaunda Suti) akiwaeleza baadhi ya viongozi wa Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii katika kuboresha mawasiliano ya serikali kwa umma. Katikati ni Kaimu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Bw. Francis Mwakapalila.


Kaimu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Bw. Francis Mwakapalila (kulia) akifurahia jambo na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene wakati alipotembelea Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ili kujionea utendaji kazi wa kitengo cha mawasiliano serikalini. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa ofisi hiyo Bw. Gerard Mwanilwa.



Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene (kulia) akisisitiza kwa  Maafisa Habari wa Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kuhusu utoaji wa taarifa kwa umma  kwa wakati. Kushoto ni Ofisa Habari wa Ofisi hiyo Bi. Evelyne Thomas. (Picha zote na Fatma Salum-MAELEZO)

No comments:

Post a Comment