Mkurugenzi
wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene akitoa pongezi kwa Mfuko wa
Pensheni wa PSPF kwa mafanikio waliopata tangu kuanzishwa kwa mfuko huo, kwenye
mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bw. Adam Mayingu akiwaeleza waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu mafanikio ya mfuko huo kwa kipindi cha miaka 15 tangu ulipoanzishwa. Kushoto ni Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF Bw. Abdul Njaidi.
Baadhi
ya watumishi wa PSPF na waandishi wa habari wakifuatilia mkutano wa mfuko huo
uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bw. Adam Mayingu akijibu maswali ya waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu tofauti za malipo ya pensheni kwa wastaafu ambapo alisema kuwa tofauti hizo zinatokana na kiwango cha mshahara na muda wa utumishi wa mwanachama. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene.
Wakurugenzi
wakionesha kwa waandishi wa habari (hawapo pichani), tuzo mbalimbali zilizotolewa
kwa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) kutokana na mafanikio yake. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa mfuko huo, Bw. Adam Mayingu, Mkurugenzi wa Fedha na Utawala, Bw. Masha Mshomba, Mkurugenzi wa
Idara ya Habari (MAELEZO), Bw. Assah Mwambene na Mkurugenzi wa Uendeshaji wa PSPF, Bi. Neema Muro. (Picha zote na Georgina Misama-MAELEZO)
Na
Fatma Salum- MAELEZO
MFUKO wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF), umeendelea kuboresha maisha ya wanachama wastaafu kwa
kuwawezesha kupata mkopo kupitia Benki ya Posta Tanzania.
Hayo
yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa mfuko huo Bw. Adam Mayingu wakati akizungumza
na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu mafanikio ya mfuko kwa
miaka 15 tangu ulipoanzishwa.
Mayingu
alifafanua kuwa mpaka sasa zaidi ya shilingi bilioni 13 zimetumika kuwakopesha
wastaafu wa PSPF wapatao 4,097 kwa lengo la kuwasaidia kwenye shughuli zao
mbalimbali za maendeleo.
“PSPF
ni mfuko wa kwanza nchini kuingia mkataba na Benki ya Posta ambapo wanachama
wastaafu wa mfuko wanaweza kupata mkopo na mpango
huu ulizinduliwa rasmi Juni 2014.”
Akieleza
zaidi mafanikio ya mfuko huo Mayingu alisema kuwa takwimu za Mamlaka ya
Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) zinaonyesha Mfuko wa
PSPF una idadi kubwa ya wastaafu na wategemezi kuliko mifuko mingine ambapo kwa
miaka kumi sasa unahudumia wastaafu na wategemezi wapatao 53,000 na kiasi cha
trilioni 2.83 zimelipwa kwa wanachama wake.
Aidha
Mayingu aliongeza kuwa PSPF wameweza kupata tuzo za kitaifa na kimataifa kutoka
kwa wadau mbalimbali wa hifadhi ya jamii ambao wametambua mchango wa mfuko huo
katika kuboresha maisha ya wanachama wake na kuchangia maendeleo ya nchi.
Naye
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene ameupongeza Mfuko wa
PSPF kwa kutoa mafao bora na kwa wakati na kuwataka waendelee kuboresha huduma
zao ili wanachama waweze kunufaika zaidi.
Akitoa
rai kwa waandishi wa habari Mwambene amesema wanapaswa kuhakikisha wanaandika
habari zitakazowasaidia watanzania kuelewa mambo mbalimbali hasa katika kipindi
hiki cha mchakato wa katiba mpya badala
ya kukazania habari zisizokuwa na tija kwa jamii.
No comments:
Post a Comment