Uharibifu uliotokea baada ya shambulizi
Takriban watu 18 wameripotiwa kuuawa katika mlipuko uliotokea sokoni mjini Maiduguri Kaskazini mwa Nigeria.
Watu walioshuhudia tukio hilo wameiambia BBC
kuwa gari lililokuwa limebeba mkaa lilipuliwa na bomu linalodhaniwa
liliwekwa ndani ya gari hilo.Hadi sasa hakuna kundi lolote la kigaidi lililokiri kufanya shambulio hilo.
Tukio hili linakuja huku ripoti ya hivi karibuni ya jeshi la Nigeria ikisema kuwa limeshambulia moja ya ngome za kundi la wapiganaji la Boko Haram.
Boko Haram wamekuwa wakifanya mashambilizi ya mara kwa mara licha ya operesheni ya kijeshi dhidi ya wapiganaji hao
No comments:
Post a Comment