TANGAZO


Monday, February 17, 2014

Polisi wamzuia mgombea Ubunge wa Chadema Jimbo la Kalenga

Polisi  wenye  silaha  mjini  Iringa,  wakijiandaa kuzuia msafara  wa mgombea  Ubunge wa Jimbo la Kalenga Iringa, kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Bi. Grace Mvanga jana kwa madai ya  kufanya maandamano yasiyo na kibali.
Mgombea  Ubunge  Jimbo la Kalenga kupitia Chadema, Bi. Grace Mvanga akipita  eneo la  kuzuizi cha Polisi baada ya kuruhusiwa kupita eneo hilo la mlima Ipogolo, mjini Iringa jana.
Polisi  Iringa  wakiwa  wameuzuia msafara  wa mgombea Ubunge Jimbo la Kalenga, Bi Grace Mvanga jana kwa madai ya kufanya maandamano bila ya kibali cha  Polisi. Mgombea huyu alizuiliwa kwa muda wa dakika  kama 20 kabla ya kuruhusiwa kupita na wafuasi wake.
Diwani  wa Kata ya Mvinjeni, Iringa  mjini, Bw. Frank Nyalusi (Chadema), kati  akiwa chini ya ulinzi wa Polisi  jana baada ya Polisi kuzuia msafara wa mgombea wa Chadema Jimbo la Kalenga Bi. Grace Mvanga eneo la mlima wa Samora, mlima wa Ipogolo mjini Iringa (Picha zote kwa hisani ya Blog ya Francis Godwin)

No comments:

Post a Comment