TANGAZO


Tuesday, December 31, 2013

Rais wa Zanzibar Dk. atoa salamu za mwaka mpya

Rais wa Zanzibar, akitoa Salamu za Mwaka mpya

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amewataka wazanzibari kuutumia mwaka ujao wa 2014 kwa kuongeza kasi, bidii na ushirikiano katika utendaji kazi ili Zanzibar iweze kufikia malengo ya maendeleo iliyojiwekea ifikapo mwaka 2015.
 
Amesema mwaka 2014 ni mwaka muhimu katika kuuweka mustakbala wa maendeleo ya Zanzibar kwa kuwa ifikapo mwaka 2015 Serikali itafanya tathmini ya utekelezaji wa mipango yake mikubwa ya maendeleo ukiwemo Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini Awamu ya Pili-MKUZA II.
 
Akitoa salamu zake za mwaka mpya wa 2014 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi amebainisha kuwa Zanzibar ikiyafikia malengo yake maendeleo sio tu kutachochea ari na hamasa kwa wananchi wake bali hata kwa washirika wake wa maendeleo na Jumuiya ya Kimataifa.

 
Kwa hiyo amewakumbusha wananchi wajibu wao wa kuitumika nchi pamoja na kuimarisha na kuendeleza umoja na ushirikiano, amani, utulivu na mapenzi baina yao.
 
Katika mnasaba huo ametoa wito kwa wananchi kuacha kufanyakazi kwa mazoea na kwa watumishi wa umma wafanye kazi kwa kutimiza wajibu wao kwa kuzingatia Sheria ya Utumushi wa Umma na Kanuni zake.
 
Dk. Shein amesema amefurahishwa sana kuona katika kipindi hiki Zanzibar inaadhimisha miaka 50 ya Mapinduzi wananchi wamekuwa wakionesha mshikamano, upendo na uzalendo bila kujali itikadi zao za kisiasa na ubaguzi.
 
Hali hiyo ameielezea kuwa ni uthibitisho wa kutosha wa mapenzi baina ya wananchi na kwa nchi yao.   
 
Kwa hiyo ametaka wananchi wazidi kuzingatia kuwa wana wajibu wa kuendelea kuyatetea, kuyalinda, kuyaenzi na kuyaendeleza Mapinduzi ya tarehe 12 Januari, 1964.
 
Katika salamu hizo Dk. Shein amewataka wananchi wajiandae pia kwa maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano yatakayofanyika mwezi April mwakani na kusisitiza kuwa Muungano huo ndio msingi wa kuimarisha udugu wa wananchi wa Zanzibar na Tanzania Bara.
 
Ametoa wito kwa wananchi kushiriki katika maonyesho ya Miaka 50 ya Mapinduzi ambayo anatarajia kuyazindua rasmi tarehe 2 Janauri, 2013 huko Beit el Raas.

1 comment:

  1. đồng tâm
    game mu
    cho thuê nhà trọ
    cho thuê phòng trọ
    nhac san cuc manh
    số điện thoại tư vấn pháp luật miễn phí
    văn phòng luật
    tổng đài tư vấn pháp luật
    dịch vụ thành lập công ty trọn gói

    Mũi kiếm trở về vị trí cũ!

    Sau một khắc, một cỗ ý cảnh bao la mờ mịt phiêu dật bay lên trong nội tâm Sở Dương, tựa hồ có người đang ngâm nga từ sâu thẳm trong lòng hắn:

    "Nhất điểm hàn quang vạn trượng mang, đồ tẫn thiên hạ hựu hà phương? Thâm mai bất cải lăng duệ chí, nhất tụ phong vân tiện thị hoàng!”

    Tạm dịch tên chiêu thức: Một điểm hàn quang vạn trượng kiếm khí - Tàn sát hết thiên hạ lại làm sao? – Chí bén nhọn chôn sâu không đổi – Gom hết phong vân để xưng hoàng!

    Tạm dịch thơ (chân thành cảmơn dịch giả A Vít tài ba đã bỏ chút thời gian hết sức quý báu của anh để hỗ trợ dịch đoạn thơ này):

    Một tia sắc lạnh vạn trượng đâm
    Nhuộm máu thiên hạ chẳng đủ tầm
    Chí sắc chôn vùi đâu giảm bén
    Phong vân tề tụ bái hùng tâm.

    Lập tức trong nội tâm Sở Dương đột nhiên xuất hiện một vài câu khẩu quyết, cùng một ít tư thế kỳ lạ. Sở Dương tâm thần chấn động, ý thức chìm vào bên trong nội tâm cẩn thận quan sát kỹ.

    ReplyDelete