TANGAZO


Friday, October 11, 2013

Wakaguzi Syria washinda tuzo ya amani ya Nobel



Wakaguzi wa silaha za kemikali Syria
Tuzo ya amani ya Nobel, mwaka huu imekwenda kwa shirika la kudhibiti silaha za kemikali duniani OPCW.
Shirika hilo kwa sasa linasimamia shughuli ya kuharibu silaha za kemikali za Syria ambazi zilitumiwa kwa mauaji ya raia wa nchi hiyo mjini Damascus mwezi Agosti.
Tangazo hili limetolewa mjini Oslo, Norway.
Kufuatia uamuzi huu, kamati ya Nobel nchini Norway imetambua kazi ya shirika hilo ambalo linaendesha shughuli ya kuharibu silaha za kemikali, kama sehemu ya azimio la kimataofa la kuharibu silaha za kemikali ambalo limesemekana kufanikiwa sana duniani.
Shirika hilo la kuzuia matumizi ya silaha za kemikali , pia husimamia azimio la silaha za kemikali duniani ambalo limefanikiwa kuharibu asimilia 80 ya zana za kemikali duniani.
Syria inatarajiwa kuwa nchi ya 131 kutia saini azimio hilo.
Nchi hiyo inasemekana kuwa na idadi kubwa ya silaha za kemikali duniani.
Tuzo ya leo kwa OPCW itaonekana kama hatua ya kutia moyo kwa shirika hilo kuendelea na kusaidia katika kutatua mgogoro wa kisiasa unaoendelea Syria
Waakilishi wa shirika hilo wataalikwa kupokea medali na tuzo ya dola milioni 1.2 za kimarekani wakati wa sherehe zitakazofanyika mwezi Disemba.

No comments:

Post a Comment