Mjini Cairo juhudi za kutafuta makubaliano ya kusitisha
mapigano baina ya Israel na Wapalestina wa Gaza zimezidishwa.
Ujumbe wa Israel umewasili Cairo na kwenda moja kwa moja kwenye mazungumzo na wakuu wa Misri.
Jumamosi Misri ilifanya mazungumzo na wakuu wa Hamas, waziri mkuu wa Uturuki na mfalme wa Qatar.
Waziri wa Mashauri ya nchi za Nje wa Israel, Avigdor Lieberman, alisema shuruti ya kwanza na ya lazima kabla ya kusitisha mapigano, ni kwamba Wapalestina lazima waache kurusha makombora kutoka Gaza kuyaelekeza Israel.
No comments:
Post a Comment