TANGAZO


Thursday, September 6, 2012

China yatuma wataalamu wake Tazara kutafiti namna ya kuboresha Reli


Mtafiti kutoka China Miao Zhong, akimuonesha Naibu Waziri Mkuu wa China, Hui Liangyu (kulia kwa aliyepeleka mkono kwenye uso), njia ya Reli ilipoanzia kwa upande wa Tanzania. Naibu Waziri Mkuu wa China alikuwa na ziara katika Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) leo asubuhi.

Waziri wa Uchukuzi, Harrison Mwakyembe, akimkaribisha Naibu Waziri Mkuu wa China Hui Liangyu, katika Stesheni ya Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA). Naibu Waziri Mkuu wa China alikuwa na ziara ya kuangalia namna Stesheni hiyo, inavyofanya kazi. Serikali ya China imetuma wataalamu kwa ajili ya kufanya utafiti wa namna ya kuiboresha Mamlaka hiyo.

 Picha ya pamoja ya ujumbe huo na Waziri Mwakyembe na timu yake, mbele ya Jengo la TAZARA leo.

Waziri wa Uchukuzi, Harrison Mwakyembe, akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani), wakati akizungumza nao katika ziara hiyo. Kulia ni Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Mhandisi Omar Chambo na kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, John Mngodo. (Picha zote na mdau wetu)

No comments:

Post a Comment