TANGAZO


Saturday, May 12, 2012

Wasudan Kusini waanza kupelekwa nyumbani

Kundi la mwanzo la Wasudan Kusini waliosubiri kwa miezi kadha kwenye kambi ya Sudan, wameanza safari ya kurudi nyumbani.
Wasudan Kusini
                     Watu kama 400, kati ya jumla ya 15,000, wanapelekwa kwa basi hadi Khartoum na kutoka hapo watasafirishwa kwa ndege hadi Juba, mji mkuu wa Sudan Kusini.
Wakuu wa Sudan walisema mwezi uliopita, kwamba watu hao ni tishio kwa usalama wa nchi.
Walipewa muda wa kuondoka nchini lakini amri hiyo baadae ilibadilishwa.
Wasudan Kusini walipoteza haki yao ya uraia baada ya Sudan Kusini kujitenga na kaskazini mwaka jana.

No comments:

Post a Comment