Breivik aliwaua watu 77
Mtu anayetuhumiwa kwa mauaji ya watu 77 nchini Norway amekanusha kutekeleza ugaidi na mauaji ya halaiki wakati wa kuanza kwa kesi yake.
Ameongeza hili lilimfanya kutekeleza mauaji ya watu 77 wengi wakiwa vijana katika shambulio la bomu mjini Oslo sawa na kuwapiga risasi vijana waliokusanyika kwa warsha ya chama cha Labour nje ya mji mkuu.
Wakati akiwasili mahakamani Breivik aliinua mkono wake. Alikaa kimya wakati akisomewa makosa yake ambapo pia majina ya waathirika wa mashambulio hayo yalisomwa. Kesi hii inatarajiwa kuchukua wiki 10 na hukumu itatolewa kabla ya mwezi Julai mwaka huu.

No comments:
Post a Comment