TANGAZO


Tuesday, January 13, 2015

Kikao cha Kamati Kuu ya CCM Mjini Unguja

Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Vuai Ali Vuai akisalimiana na Makamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pia Mjumbe wa Kamti Kuu ya CCM Taifa Dk. Mohammed Gharib Bilali wakati alipowasili Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja leo katika Kikao cha kawaida cha Kamati Kuu ya CCM Taifa chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, (Picha zote na Ikulu)
Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein (katikati) akisalimiana na Mjumbe wa Sekretarieti ya Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya Taifa Haji Mkema mara alipowasili Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja leo, alipohudhuria katika kikao cha kawaida cha siku moja cha Kamati Kuu ya CCM Taifa. Wapili kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai na kushoto ni Katibu Mkuu wa CCM Taifa Abdulrahman Kinana.
Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akibadilishana mawazo na Katibu Mkuu wa CCM Taifa Abdulrahman Kinana katika viwanja vya Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja leo walipohudhuria katika Kikao cha kawaida cha siku moja cha Kamati Kuu ya CCM Taifa.
Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete   akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai leo alipofika Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja  akihudhuria Kikao cha kawaida cha Kamati Kuu ya CCM Taifa (katikati) Katibu Mkuu wa CCM Taifa Abdulrahman Kinana.
Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete   akisalimiana na wazee wa Chama cha Mapinduzi alipofika Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja leo akihudhuria Kikao cha kawaida cha Kamati Kuu ya CCM Taifa.
Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) alipokuwa akiongoza Kikao cha kawaida cha Kamati Kuu ya CCM Taifa kilichofanyika leo katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja (kushoto) Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein.
Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) akiongoza Kikao cha Kamati Kuu ya CCM Taifa kilichofanyika leo katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja,

No comments:

Post a Comment