TANGAZO


Thursday, March 22, 2018

WAZIRI WA ULINZI WA ISRAEL AVIGDOR LIBERMAN ATEMBELEA TAASISI YA MOYO YA JAKAYA KIKWETE (JKCI)

Waziri wa Ulinzi wa Israel, Mhe. Avigdor Liberman akimpa zawadi mtoto aliyefanyiwa upasuaji wa moyo nchini Israel alipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jana huku Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee  na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akishuhudia. Tangu mwaka 2015 JKCI kwa kushirikiana na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) ya nchini Israel wanafanya kambi maalum za matibabu ya moyo kwa watoto. (Picha zote na JKCI)
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee  na Watoto, Mhe.Ummy Mwalimu 
na Waziri wa ulinzi wa Israel Mhe. Avigdor Liberman  wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto na wazazi wao ambao walifanyiwa upasuaji wa moyo nchini Israel.  Mhe. Liberman  alitembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jana kwa ajili ya kuona ushirikiano ulipo kati ya JKCI na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) ya nchini Israel ambao kwa kushirikiana wanafanya kambi maalum za matibabu ya moyo kwa watoto ambapo watoto wanaokutwa na matatizo yanayohitaji matibabu ya hali ya juu wanatibiwa nchini humo bila malipo.  
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee  na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akimpa zawadi ya kitenge  Waziri wa ulinzi wa Israel Mhe. Avigdor Liberman alitembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jana kwa ajili ya kuona ushirikiano ulipo kati ya JKCI na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) ya nchini Israel ambao kwa kushirikiana wanafanya kambi maalum za matibabu ya moyo kwa watoto ambapo watoto wanaokutwa na matatizo yanayohitaji matibabu ya hali ya juu wanatibiwa nchini humo bila malipo. 
Waziri wa Ulinzi wa Israel, Mhe. Avigdor Liberman akimpa zawadi mtoto aliyefanyiwa upasuaji wa moyo nchini Israel alipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jana huku Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee  na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akishuhudia. Tangu mwaka 2015 JKCI kwa kushirikiana na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) ya nchini Israel wanafanya kambi maalum za matibabu ya moyo kwa watoto.  
Waziri wa Ulinzi wa Israel Mhe. Avigdor Liberman  akisaini kitabu cha wageni alipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jana kwa ajili ya kuona ushirikiano ulipo wa matibabu ya moyo kwa watoto, kusomesha madaktari na wauguzi kati  ya JKCI na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) ya nchini Israel. Kulia ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee  na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu. 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee  na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu na Waziri wa ulinzi wa Israel Mhe. Avigdor Liberman  wakiwa katika picha ya pamoja na madaktari pamoja na wauguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambao walisoma nchini Israel kwa udhamini wa Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) ya nchini humo.

No comments:

Post a Comment