TANGAZO


Friday, March 30, 2018

Tetesi za soka Ulaya Ijumaa 30.03.2018: Isco ameendelea kutafutwa, Robert Lewandowski naye anaitaka Madrid

Isco

Image captionManchester City inatuma kusaini mkataba na mchezaji wa kiungo cha kati wa Real Madrid Mhispania Isco
Manchester City wanaamini wanaweza kusaini mkataba na mchezaji wa kiungo cha kati wa Real Madrid Mhispania Isco msimu huu wa majira ya joto. Mkataba kwa ajili ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 unaweza kuwa wa thamani ya Euro milioni 75. (Mirror)
Mchezaji wa kiungo cha kati wa Ubelgiji Mousa Dembele, mwenye umri wa miaka 30, hatasaini mkataba mpya na Tottenham kabla ya Kombe la Dunia la mwaka huu, na hivyo kuibua maswali kuhusu mustakabali wake katika klabu hiyo. (Telegraph)
Mshambuliaji wa Bayern Munich Robert Lewandowski, mwenye umri wa miaka 29, atawasilisha maombi yake ya kutaka kuhamia Real Madrid msimu huu wa majira ya joto. Mchezaji wa Chelsea mwenye umri wa miaka 25 na mchezaji wa kimataifa wa Uhispania Alvaro Morata ni mmoja wa washambuliaji ambao Bayern Munich inamtaka kwa ajili ya kuchukua nafasi ya Pole iwapo watampoteza. (AS - in Spanish)
Winga wa Crystal Palace Andros TownsendHaki miliki ya pichaHUW EVANS PICTURE AGENCY
Image captionWinga wa Crystal Palace Andros Townsend anasema kuwasaidia Eagles kuepuka kushuka daraja ni suala analolipa kipaumbele zaidi.
Mchezaji wa kiungo cha kati wa Paris St-Germain midfielder Hatem Ben Arfa ametangaza kuwa ataondoka katika Ligi kuu ya Ufaransa mwisho wa msimu. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31, raia wa Ufaransa, amekuwa na uhusiano na Leicester City. (Sun)
Meneja wa Watford Javi Gracia amemkosoa Abdoulaye Doucoure, mwenye umri wa miaka 25, kwa kukataa kuhama katika msimu huu wa majira ya joto, huku Manchester United Tottenham, Liverpool na Arsenal kwa pamoja wakimthamanisha mchezaji huyo wa kiungo cha kati kwa kiwango cha Euro milioni 40. (Mail)
Mmiliki wa Newcastle United Mike AshleyHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMmiliki wa Newcastle United Mike Ashley ataanza mkakati wake wa kuuza klabu hiyo
West Ham wana imani ya kusaini mkataba na nahodha wa timu ya Urusi Fyodor Smolov. Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 28, anayechezea klabu yake ya soka ya Krasnodar, anaweza kuhama kwa malipo ya Euro milioni £15m. (Mirror)
Mmiliki wa Newcastle United Mike Ashley ataanza mkakati wake wa kuuza klabu hiyo mara tu watakapohakikishiwa kwamba watafanikiwa kusalia Ligi ya Premia. (Telegraph)
Ligi ya Premia inatarajia kuanza kujaribu kupunguza idadi ya waamuzi katika mchakato wa video ya usaidizi wa maamuzi ya marefarii (VAR), badala ya kutegemea video rasmi bila kumuhusisha mtu yeyote. (Times)
Rhian Brewster
Image captionKijana Rhian Brewster mchezaji wa timu ya England ya vijana walio chini ya umri wa miaka 17 anasakwa na timu za Ligi ya Primia na nyingine
Manchester United imeanzisha msimu wa kupunguza gharama za tiketi za kuangalia michezo yake kwa vijana wenye umri wa miaka 16 hadi 25 kwa lengo la kuboresha uwepo wa watazamaji katika Old Trafford. (Telegraph)
Liverpool itaanzisha mazungumzo na kijana wa kikosi cha England kilichochukua kombe la dunia la vijana walio chini ya umri wa miaka 17 Rhian Brewster. Klabu mbali mbali za Ligi ya Primia na nyingine zimeonyesha nia ya kumtaka na mkataba wake wa sasa unamalizika katika msimu wa majira ya joto. (Sun)
Meneja wa Manchester City Pep Guardiola amekosolewa na daktari wa zamani wa Bayern Munich, ambaye anasema kuwa anaweka mbele mafanikio mbele zaidi ya afya ya wachezaji. (Mail)
Winga wa Crystal Palace Andros TownsendHaki miliki ya pichaHUW EVANS PICTURE AGENCY
Image captionWinga wa Crystal Palace Andros Townsend anasema kuwasaidia Eagles kuepuka kushuka daraja ni suala analolipa kipaumbele zaidi.
Meneja wa timu ya Ubelgiji Roberto Martinez amemuonya mchezaji wa safu ya ulinzi ya Tottenham Toby Alderweireld mwenye umri wa miaka 29, kwamba nafasi yake katika kikosi cha Kombe la dunia imo mashakani ataendelea kutopendelewa na Mauricio Pochettino. (Guardian)
Winga wa Crystal Palace Andros Townsend, mwenye umri wa miaka 26, anasema kwamba licha ya kwamba ananuia kurejeshwa na England, kuwasaidia Eagles kuepuka kushuka daraja ni suala analolipa kipaumbele zaidi. (Mirror)
Meneja wa Cardiff City Neil Warnock amejipapatia jina la mtu wenye roho nyepesi, akiongeza kuwa: "Ninalia sana ninapotazama kipindi cha televisheni cha - I watch Call the Midwife." (Mail)
Lee Bowyer anasema alikuwa mshindani sana kama mchezaji wakati fulani lakini anataka sana kujulikana kama meneja anayewajali wachezaji Charlton. (Express)
Mchezaji wa safu ya kati wa Arsenal mFaransa Laurent Koscielny, mwenye umri wa miaka 31, ameanza kufanya yoga kwa ajili ya kurefusha muda wake kama mchezaji wa kulipwa. (Sun)

No comments:

Post a Comment