TANGAZO


Thursday, April 27, 2017

WAZIRI UMMY ASISITIZA WANAFUNZI WANAOPATA UJAUZITO WAENDELEE NA MASOMO

Mkuu wa Chuo cha DUCE Profesa William Anangisye akihutubia jopo la Wadau na wanafunzi katika mkutano wa masuala ya Usawa na huku akisisitiza wazazi na walezi kuwatia moyo wanafunzi wa kike kupenda  masomo ya sayansi ili kupata  wanasayansi wanawake nchini. 
Profesa Rwekaza Mukandala Makamu Mkuu wa Chuo kikuu cha Dar Es Salaam akihutubia wadau na wanafunzi  waliojitokeza katika mkutano wa kwanza wa masuala ya Jinsia na Usawa yaliyofanyika katika chuo kikuu cha Uwalimu DUCE jijini Dar Es Salaam. 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na watoto Mh. Ummy Mwalimu akimuwakilisha Makamu wa Raisi Bi Samia Suluhu Hassan katika ufunguzi wa  mkutano wa kwanza wa Masuala ya Usawa wakijinsia  ulioandiliwa na Chuo Cha Ualimu (DUCE) jijini Dar Es salaam. 
Wadau wa Masuala ya Usawa wa kijinsia wakifuatilia kwa ukaribu ujumbe uliokuwa ukitolewa na Mh.Ummy Mwalimu Waziri wa Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na watoto aliyekuwa akimuwakilisha Makamu wa Raisi Bi Samia Suluhu Hassan katika viunga vya Chuo cha Uwalimu DUCE jijini Dar Es Salaam. 
Picha ya pamoja ya wadau wa masuala ya Usawa wakijinsia katika mkutano wa kwanza wa masuala ya Usawa wakijinsia uliowakutanisha kujadili na kuhamasisha  juu ya kumlinda mtoto wa kike ili apate Elimu sawa kama ile apatayo mtoto wakiume katika jamii yetu.

WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesisitiza kuwa wanafunzi wa kike wanaopata mimba wakiwa mashuleni waendelee na masomo yao ili kufikia malengo walioyanayo nchini.

Ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kwanza wa maswala ya kijinsia ulioandiliwa na Chuo Cha Ualimu (DUCE) alipomuwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri8 ya Muungano waq Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo jijini Dar es salaam.

“Tunapokataza watoto wa kike wasiendelee na masomo pindi wanapopata ujauzito wakiwa mashuleni  tunawaadhibu watoto wa masikini washindwe kutimiza malengo yao kwa wakati waliotarajia”alisema Waziri Ummy.

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa anaunga mkono uamuzi wa  Rais wa Tanzania Dkt. Jonh Pombe  Magufuli kwa  kutoa elimu bure nchini kwani kunaongeza idadi ya watoto wa kike  kuwepo mashuleni tofauti na kipindi cha nyuma.

Mbali na hayo Waziri Ummy ametoa wito kwa wazazi kuwahamasisha watoto wao wa kike kupenda masomo ya sayansi ili kukuza rasilimali watu katika kujenga uchumi unaotokana na viwanda nchini.


Kwa upande wa Mkuu wa Chuo cha DUCE Prof. William Anangisye amesema kuwa lengo la  mkutano huo ni kuleta chachu ya kuwatia moyo wanafunzi wa kike kupenda  masomo ya sayansi ili kupata  wanasayansi wanawake nchini.

No comments:

Post a Comment