Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Nuru Halfan Mrisho, pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Sofia Mjema wakiokota baadhi ya uchafu katika kaburi la nguli mpigania Uhuru wa Tanganyika, Hayati Kaluta Amri Abeid Kaluta walipozuru kaburi hilo, katika kuadhimisha siku ya Afrika leo, jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni mtoto wa tano wa hayati Sheikh Kaluta Bw. Amiri Kaluta Amri Abedi na kulia ni Naibu Meya Bw. Salum Faisal.
Mtoto wa tano wa hayati sheikh Kaluta Bw. Amiri Kaluta Amri Abedi (watatu kulia) akiongoza dua ya kumuombea baba yake hayati sheikh Kaluta Amri Abeid wakati ujembe kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ulipozuru katika kaburi la nguli huyo kuadhimisha siku ya Afrika leo Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Sofia Mjema (kushoto mbele) akizungumza wakati ujumbe kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ulipozuru katika kaburi la nguli mpigania Uhuru wa Tanganyika Hayati Kaluta Amri Abeid Kaluta kuadhimisha siku ya Afrika leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara hiyo Bibi. Nuru Halfan Mrisho.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Nuru Halfan Mrisho (kulia) akizungumzia siku ya Afrika alipozuru katika kaburi la nguli mpigania Uhuru wa Tanganyika Hayati Kaluta Amri Abeid Kaluta kuadhimisha siku ya Afrika leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto mbele ni Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Sofia Mjema.
Katibu Mtendaji Baraza la Kiswahili Taifa Dkt. Suleimani Sewangi (mwenye miwani) akisoma tawasifu ya hayati Sheikh Kaluta Amri Abeid Kaluta wakati ujumbe kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ulipozuru katika kaburi la nguli huyo kuadhimisha siku ya Afrika leo Jijini Dar es Salaam.
Bw. Kassim Amotile (mwenye miwani) akigani Shairi lililoandikwa na marehemu Mathias Mnyampala mwaka 1964 wakati wa kifo cha hayati Sheikh Kaluta Amri Abeid Kaluta na kulipa jina la Kifo cha Sheikh Abeid, Pengo kuu kwa Taifa wakati ujumbe kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ulipozuru katika kaburi la nguli huyo kuadhimisha siku ya Afrika leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Sofia Mjema na wapili kulia ni Naibu Katibu Mkuu kutoka Wizara hiyo Bibi Nuru Halfan Mrisho.
Na
Genofeva Matemu – Maelezo
Tarehe:
25/05/2016
MAMLAKA ya
Halmashauri ya Wilaya ya Temeke imeagizwa kuandaa siku maalumu itakayowawezesha
wananchi wakiwemo wanafunzi kuzuru kaburi la nguli mpigania uhuru wa Tanganyika
Hayati Kaluta Amri Abeid Kaluta na kulifanya kuwa eneo la kiutamaduni na
kihistoria.
Rahi hiyo
imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Sophia Mjema alipoongozana na ujumbe
kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuzuru kabuli la nguli
huyo katika kuadhimisha siku ya Afrika leo Jijini Dar es Salaam.
“Nguli kama
Hayati Abeid Kaluta ni watu wenye historia kubwa katika kupigania uhuru wa
Tanganika ni vyema Uongozi wa Wilaya ya Temeke kuandaa siku maalumu na kuialika
familia yake kuzuru kaburi hili na kupata historia ya Tanganyika kupitia nguli
huyu” alisema Mhe. Mjema.
Aidha Mhe.
Mjema ametoa rai kwa wakuu wa wilaya zote nchini kutambua mashujaa waliopigania
uhuru wa Tanganyika kwa kutambua shule na mitaa ama maeneo yanayotumia majina
ya mashujaa hao kwa kuwaenzi na kusambaza historia zao kwa jamii
inayowazunguka.
Akizungumza
wakati wa ziara hiyo Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na
Michezo Bibi. Nuru Halfan Mrisho amesema kuwa Wizara imeamua kuzuru kaburi la
Hayati Kaluta Amri Abeid kama njia ya kuenzi mchango wa shujaa huyo na
kuhabarisha umma historia ya shujaa Abeid ambaye walio wengi hawamjui na
hawafahamu mchango alioutoa kwa nchi
hii.
Bibi. Mrisho
amesema kuwa uwepo wa kaburi la Hayati Kaluta Amri Abeid ni fursa ya kipekee ya
kutangaza utalii wa kiutamaduni na eneo la kihistoria katika Wilaya ya Temeke.
Hayati Sheikh
Amri Abeid Kaluta alizaliwa mwaka 1924 Mkoani Kigoma na kufariki dunia mwaka
1964 huko Boni nchini Ujerumani. Ametoa mchango mkubwa katika Taifa kwa kuwa
mwanaharakati mpigania uhuru kwa kutumia silaha ya mashairi, ni mkuzaji na
muenezaji wa Utamaduni, utanzu wa fasihi na alikuwa Sheikh Mkuu wa kidini
dhehebu la Ahmadiyya.
No comments:
Post a Comment