Na Frank Shija,
MAELEZO
Wanafunzi na
vijana wakitanzania kuendelea kunufaida na usafiri wa njia ya anga kwa gharama
nafuu kupitia Kampuni ya Sta Travel yenye maskami yake mtaa wa mtendeni manispa
ya Ilala jijini Dar es Salaam.
Hayo
yamebainishwa na Meneja uendeshajji wa Kampuni hiyo Abass Takim alipokuwa
akizungumza na mwandishi wa habari hii ofisini kwake jana.
Takim amesema
kuwa watanzania wanaosoma elimu ya juu nje ya nchi wanayofurusa ya kunufaiki na
huduma zaokwa kuwaunganisha na usafiri wa gharama ndogo zenye punguzo maalum za
kusafiri wakati wa kwenda na kurudi kutoka masomoni katika nchi wanazosomea.
Takkim amesema
kuwa taasisi yao imekuwa msaada mkubwa kwa Watanzania wanaopata fursa ya kusoma
nje ya nchi kwani wanatoa huduma ya usafiri ikiwa na punguzo maalum la gharama
za usafiri ili waweze kumudu gharama hizo, ambapo huduma hiyo ya usafirishaji
wa wanafunzi kwa gharama nafuu inaenda sambamba na huduma za malazi kwa gharama
nafuu wakati wa kwenda na kurudi,Bima ya safari na Kitambulisho cha Kimataifa cha Mwanafunzi
Aliongeza kuwa
mpaka sasa Taasisi yake imetoa huduma ya hiyo kwa watanzania wengi hasa
wanafunzi wanaoenda kusoma katika vyuo vya Kuala Lumpar Malyasia, London
Uingereza, na Guangzhou China.
Aidha Abbas
alisema kuwa pamoja na kutoa huduma hiyo kwa watanzania kumekuwa na changamoto
katika upatikanajji wa Viza kwa wateja wao na kupelekea kujitokeza kwa
usumbufu, hata hivyo Sta Travel imekuwa ikijitahidi kuwasaidia wateja wake ili
wakamilishe taratibu zao kwa wakati.
Sta Travel niasasi
inayojihusisha na utoaji wa huduma ya kusafirisha wanafunzi kwa gharama nafuu ikiwa
na punguzo kwa lengo la kuwasaidia watanzania kufikia ndoto zao bila kuwapo na
kikwazo.
Katika
kuhakikisha inafikia wateja wake kwa urahisi zaidi Sta Travel imefungua zaidi
ya matawi 400 katika nchi 100 dunia kote ambapo kwa Tanzania ofisi zake
zinapatikana katika mtaa wa Mtendeni, Kisutu (Posta),Takims Holidays / STA
Travel Partner mkabala na Supermarket ya Shrijee jijini Dar es Salaam unaweza
pia kuwasiliana nao kupitia simu namba +255 758 828384/85 au tembelea tovuti
yao http://www.escape-tanzania.com/
No comments:
Post a Comment