Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Bw. Shabani Mwinjaka akienda kukagua moja ya karakana za shirika la reli Tanzania (TRL) alipofanya ziara yake Tanzania leo jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Bw. Shabani Mwinjaka akitoka kukagua moja ya karakana za shirika la reli Tanzania (TRL), alipofanya ziara yake Tanzania leo jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Bw. Shabani Mwinjaka akikagua moja ya karakana za shirika la reli Tanzania(TRL) alipofanya ziara yake Tanzania leo jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Bw. Shabani
Mwinjaka akisisistiza jambo kwa wafanyakazi wa shirika la reli
Tanzania(TRL) alipofanya ziara yake
Tanzania leo jijini Dar es Salaam. (Picha zote na Ally Daud - Maelezo)
Na Ally Daud-Maelezo
Dar es Salaam
30/12/2015
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Shabani Mwinjaka amefanya ziara katika
Shirika la Reli Tanzania (TRL)ili kuhakikisha ufanyaji kazi wa shirika hilo
linaendana na kasi yaRais wa awamu ya tano Mh. John Pombe Magufuli.
Katika ziara hiyo Bw. Mwinjuko alikagua karakana za
shirika hilo ili kuona utendaji wake na kusisitiza ukarabati wa mebehewa
yaliyobaki kumaliziwa ndani ya siku 30.
Hata hivyo katibu
huyo amestushwa na habari ya kuanguka kwa mabehewa 50 ya mafuta
yaliyokuwa yanajaribiwa huko
Tanga.
“Nimestushwa na taarifa ya kuanguka kwa mabehewa 50
ya mafuta katika majaribio baada ya kujazwa maji ,yangekuwa yana mafuta ingekua
hasara kubwa kwa Tanzania hivyo nataka tatizo hilo lishughulikiwe haraka
iwezekanavyo kunusuru mabehewa yaliyobaki .”alisema Mwinjaka.
Mbali na hayo Bw.Mwinjaka alisema kwamba reli ambazo
zimehifadhiwa katika karakana hizo ziondolewe na zikamalizie ujenzi wa reli
ambazo hazijaisha kuliko kukaa bila ya
matumizi huku kukiwa na shida ya mataaluma hayo.
Kwa upande wa Mkurugenzi wa Shirika la Reli Tanzania
Bw.Elias Mshana amesema kwamba wapo katika mchakato wa kumalizizia ukarabati wa
mabehewa yaliyobaki pamoja na marekebisho ya reli zilizoharibika na mpaka 31
Desemba mwaka huu zitakua zimetengemaa.
“Tunatarajia mpaka tarehe 31 Decemba mwaka huu
tutakua tumemaliza kukarabati mabehewa na reli zilizoharibika ili zianze
kutumiwa rasmi ili kuleta maendeleo katika Nchi” Alisema Bw. Mshana.
No comments:
Post a Comment